Skip to main content

KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AICHANA CHADEMA TUNDUMA-MOMBA

1Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana jioni ya leo, amefanya mkutano mkubwa wa hadhara mjini Tunduma, ambao umehudhuriwa na maelfu ya wananchi. Katika mkutano huo uliofabnyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Mwaka, Kinana aliambatana na majenbe ya Chama cha Mapinduzi  , Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro, Katika mkutano huo Kinana amesema wananchi kuikosoa CCM sio kosa kwani Chama hicho kimeingia mkataba na wananchi pale kilipopewa ridhaa ya kuongoza nchi ili kutekeleza ilani yake ya uchaguzi na ni haki ya mtu yeyote wakiwemo wapinzani ili kujua maendeleo yao, Amesema CCM haitakubali kuona ukiritimba na umangimeza wa baadhi ya watendaji  Serikalini  unakwamisha maendeleo ya wananchi, ameongeza kuwa kazi ya CCM ni kutenda tu. na kazi ya wapinzani ni kusema maneno matupu.PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-TUNDUMA-MOMBA 2Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma. 3Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro akisalimia maelefu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano huo. 4Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa amebebwa juujuu na wananchi waliohudhuria kwenye mkutano huo. 5Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro akisakata muziki na wakina mama wana CCM kabla ya kuanza kwa mkutano huo. 6Wananchi wakisakata muziki kabla ya kuanza kwa mkutano.

Comments