Skip to main content
KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AICHANA CHADEMA TUNDUMA-MOMBA
Katibu
Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana jioni ya leo, amefanya mkutano
mkubwa wa hadhara mjini Tunduma, ambao umehudhuriwa na maelfu ya
wananchi. Katika mkutano huo uliofabnyika kwenye Uwanja wa Shule ya
Msingi Mwaka, Kinana aliambatana na majenbe ya Chama cha Mapinduzi ,
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Katibu wa NEC Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro, Katika mkutano huo Kinana
amesema wananchi kuikosoa CCM sio kosa kwani Chama hicho kimeingia
mkataba na wananchi pale kilipopewa ridhaa ya kuongoza nchi ili
kutekeleza ilani yake ya uchaguzi na ni haki ya mtu yeyote wakiwemo
wapinzani ili kujua maendeleo yao, Amesema CCM haitakubali kuona
ukiritimba na umangimeza wa baadhi ya watendaji Serikalini unakwamisha
maendeleo ya wananchi, ameongeza kuwa kazi ya CCM ni kutenda tu. na
kazi ya wapinzani ni kusema maneno matupu.PICHA NA KIKOSIKAZI CHA
FULLSHANGWE-TUNDUMA-MOMBA
Katibu
wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia maelfu ya wananchi
waliojitokeza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa
shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma.
Katibu
wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro akisalimia
maelefu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano huo.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa amebebwa juujuu na wananchi waliohudhuria kwenye mkutano huo.
Katibu
wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro akisakata
muziki na wakina mama wana CCM kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Wananchi wakisakata muziki kabla ya kuanza kwa mkutano.
Comments
Post a Comment