Skip to main content

Shilingi bilioni 43 `Mabilioni ya JK`zarejeshwa


Mary Nagu(5)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya serikali ya awamu ya nne jijini Dar es Salaam jana.

Shilingi bilioni 43 kati ya bilioni 50.03 za mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuongeza ajira, maarufu kama “Mabilioni ya JK” zimerejeshwa kutoka kwa wajasiriamali 74,701 waliokopeshwa na serikali kwa awamu mbili tofauti katika mikoa yote nchini.
Fedha hizo zilitolewa kwa utaratibu wa serikali kutoa dhamana ya mikopo kwenye benki za CRDB, NMB, Community na Benki ya Posta.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk. Mary Nagu, alisema hayo katika mkutano kati yake na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya serikali ya awamu ya nne katika maeneo yanayohusu Idara ya Maendeleo ya Sekta binafsi, Uwekezaji na Uwezeshaji, jijini Dar es Salaam jana.
Alisema wananchi waliokopeshwa fedha hizo wamepiga hatua kubwa kiuchumi na kwamba, serikali inaendelea kukusanya marejesho ya madeni ya mikopo iliyochukuliwa.
Kwa mujibu wa Waziri Nagu, hali hiyo ni uthibitisho kwamba Watanzania ni watu wanaoaminika pale wanapofuatiliwa.
Kutokana na hali hiyo, alisema serikali hivi sasa inafanya tathmini kuangalia uwezekano wa kuendelea kuwakopesha wananchi wengine ili kuwakomboa kiuchumi. 
 
Aidha, alisema serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji ili kuhamasisha na kuvutia miradi ya uwekezaji nchini.
Alisema serikali itaendelea kuhamasisha uwekezaji nchini kwa kuboresha na kutekeleza sera na sheria zitakazovutia uwekezaji kwani inasaidia kuongeza pato la taifa na kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania.
Waziri Nagu alisema kutokana na jitihada za serikali za kuweka mazingira wezeshi na kuhamasisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, idadi na thamani ya miradi iliyoidhinishwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) imeendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka.
“Na hii inasaidia kuongeza pato la taifa na kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania,” alisema Dk. Nagu.
Alisema ili kuendelea kuboresha sera na sheria za uwekezaji ziendane na mazingira na mahitaji ya uwekezaji, serikali imeshakamilisha maandalizi ya taarifa ya mapitio ya sera zinazohusu uwekezaji.
Kwa mujibu wa Waziri Nagu, maandalizi hayo yalifanyika kwa kutumia mfumo wa kutathmini sera za uwekezaji unaotumiwa na Shirika la Kimataifa la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo (OECD).
Alisema nia ya serikali ni kuhakikisha sekta binafsi inachukua nafasi yake kwa kuwa ni moja ya misingi ya uchumi wa soko, hivyo akasema hakuna Mtanzania mwenye uwezo atakayekataliwa kuwekeza ili kukuza uchumi wa nchi. 
CHANZO: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Tazama picha za utupu ya Mwimbaji wa nyimbo za injili

Hili nalo ni tukio la kushitua baada ya msanii wa nyimbo za injiri kuamua kuanika picha zake za utupu kunako mitandao ya kijamii tukio hili limetokea hivi karibuni Nchini Nigeria Baada ya mwimbaji wa nyimbo za injiri kuweka piha na video kwenye mtandao anajulikana kwa jina la Maheeda  I doubt if this Naija female singer called Maheeda could still be described as a gospel singer giving her acts in recent times, especially in the social media. Her latest show of shame is posting videos of herself in the n*de while taking her bath. Check out more of her craze below:

Tazama Pichaz 14 za Kilimanjaro Stars ilivyowasili uwanja wa ndege wa JKIA Dar baada ya kutolewa Challenge

Timu ya taifa ya  Tanzania  bara  Kilimanjaro Stars  imewasili  Dar Es Salaam  December 2 ikiwa ni siku mbili zimepita toka itolewe na timu ya taifa ya  Ethiopia  katika michuano ya mataifa ya  Afrika Mashariki  na kati maarufu kama  CECAFA Senior Challenge Cup 2015 .  Kilimanjaro Stars  itolewa na  Ethiopia  katika hatua ya robo fainali kwa mikwaju ya penati 4-3 baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya goli 1-1. Naomba nikusogeze pichaz 15 za timu ya taifa ya  Tanzania  Bara  Kilimanjaro Stars  ikiwasili uwanja wa ndege Dar Es Salaam. Himid Mao baada ya kuwasili Nahodha wa Kilimanjaro Stars John Bocco baada ya kutua Dar akielekea katika basi. John Bocco na kocha mkuu na msaidizi wake wakizungumza jambo Shomari Kapombe ndani ya basi la timu ya Taifa Hassan Kessy akipanda basi la Stars Mshauri wa Kilimanjaro Stars na kocha wa Taifa Stars Charles Boniface Mkwasa aki...