Skip to main content

Mbunge wa CHADEMA kanusurika kwenye ajali ya hii Helicopter leo July 07 2015.

Taarifa ilianza kuenea jioni ya July 07 2015 kwenye kuhusu ajali ya Helicopter iliyokua imebeba Wanachadema mbalimbali akiwemo mbunge Arumeru Mashariki Joshua Nassari.

Kwenye ukurasa wa Twitter wa CHADEMA zimewekwa post kwamba Mbunge Joshua Nassari ndiye aliyepata ajali hiyo ya Helicopter, amepelekwa Hospitali kwa ajili ya matibabu pamoja na rubani na watu wengine ambao hawajatajwa, ni baada ya kunusurika.

Moshono media inaendelea kufatilia zaidi na chochote kitakachopatikana iwe usiku au mchana utakipata hapahapa.

 

Mkiti Mbowe ametoa pole, kuwatakia uponaji wa haraka majeruhi wote; Mbunge, viongozi wa chama na rubani @jjmnyika @halimamdee @salum_mwalimu

— CHADEMA MEDIA (@ChademaMedia) July 7, 2015

“Tukiwa kikaoni tumepokea taarifa za ajali ya chopper ikiwahusisha Mbunge, Viongozi wa Chama na rubani,” @jjmnyika @halimamdee @JoeMugasa

— CHADEMA MEDIA (@ChademaMedia) July 7, 2015

Ni jambo la kumshukuru Mungu Mh.Nassari amenusurika kwenye Ajali hii Mbaya

Comments