Skip to main content

Magufuli Aitaka TRA Kutoa Mashine za EFDs Bure.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli, ameishangaa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kwa kutogawa bure Mashine za EFDs, na wao kubaki na kazi ya kukusanya mapato.

Akizungumza katika mkutano wa wafanyabiashara na wawekezaji jana jijini Dar es Salaam, ulioandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) na Baraza la Biashara la Taifa (TNBC), alisema muda uliopotea na kodi ambayo haikukusanywa wakati wa mvutano na wafanyabiashara ungetosha kununua mashine mpya na kuwagawia.

“Kama mnajua mashine hizi ni halali na ni zenu, wapeni bure kazi yenu iwe ni kukusanya kodi, ni hesabu rahisi sana isiyohitaji kwenda chuo kikuu kuwa muda uliopotea na fedha hazifiki bilioni 12 zingetosha kununua na iwe kazi ni kukusanya kodi,” alisema.

Awali katika salamu zake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara, Jonson Minja, alimpongeza rais kwa kazi kubwa aliyofanya Bandarini na TRA kwa kuwa imewezesha kodi kukusanywa kwa usahihi na kwamba kipindi cha nyuma fedha nyingi zilipotea, kutokana na mfumo wa ukusanyaji kodi kutowekwa wazi.

Aidha, alisema mashine za EFDs zitatumika kwa wafanyabiashara wote mwakani, kwa kuwa changamoto zilizosababisha mvutano baina yao na serikali zimemalizika.

Aidha, alimtaka rais kufuatilia kwa karibu ukwepaji kodi katika sekta isiyo rasmi na kwamba kukiwa na mipango madhubuti serikali itaweza kupata kodi kwa wananchi wote.

“Kasi ya rais inatupa matumaini makubwa sana, tunachoweza kusema, Mungu akubariki akupe hekima na nguvu...tunaomba uimarishe viwanda vya kati na vidogo ili malighafi zisisafirishwe kwenda nje, bidhaa ambazo zitasaidia kukuza uchumi na kuimarisha shilingi dhidi ya Dola ya Marekani,” alisema.

Tangu mwaka juzi kulikuwa na mvutano mkali baina ya wafanyabiashara na TRA, ambao waligoma kutumia mashine hizo hadi serikali itakaposhughulikia kero zao ikiwamo bei ya mashine, utitiri wa kodi, ukwepaji kodi na urasimu uliopo.

Wafanyabiashara kwa umoja wao waliitisha mgomo nchi nzima na kumekuwa na mazungumzo ya mara kwa mara na serikali, ambayo wakati mwingine hayakufikia ukingoni, hatua iliyofanya baadhi ya viongozi wa wafanyabiashra kukamatwa.

Minja alikamatwa na Polisi mkoani Dodoma mwaka jana, na kuswekwa ndani, jambo lililofanya wafanyabiashara kuitisha mgomo wa siku tatu hadi serikali itakapoeleza alipo kiongozi wao.

Baadaye ilibainika anashikiliwa na Polisi mkoani humo, na alipandishwa mahakama ya mkoa na kusomewa mashtaka ya kuchochea mgomo wa wafanyabiashara nchini.

Baadaye mahakama ya mkoa ilimuachia huru kiongozi huyo.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Tazama picha za utupu ya Mwimbaji wa nyimbo za injili

Hili nalo ni tukio la kushitua baada ya msanii wa nyimbo za injiri kuamua kuanika picha zake za utupu kunako mitandao ya kijamii tukio hili limetokea hivi karibuni Nchini Nigeria Baada ya mwimbaji wa nyimbo za injiri kuweka piha na video kwenye mtandao anajulikana kwa jina la Maheeda  I doubt if this Naija female singer called Maheeda could still be described as a gospel singer giving her acts in recent times, especially in the social media. Her latest show of shame is posting videos of herself in the n*de while taking her bath. Check out more of her craze below:

Tazama Pichaz 14 za Kilimanjaro Stars ilivyowasili uwanja wa ndege wa JKIA Dar baada ya kutolewa Challenge

Timu ya taifa ya  Tanzania  bara  Kilimanjaro Stars  imewasili  Dar Es Salaam  December 2 ikiwa ni siku mbili zimepita toka itolewe na timu ya taifa ya  Ethiopia  katika michuano ya mataifa ya  Afrika Mashariki  na kati maarufu kama  CECAFA Senior Challenge Cup 2015 .  Kilimanjaro Stars  itolewa na  Ethiopia  katika hatua ya robo fainali kwa mikwaju ya penati 4-3 baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya goli 1-1. Naomba nikusogeze pichaz 15 za timu ya taifa ya  Tanzania  Bara  Kilimanjaro Stars  ikiwasili uwanja wa ndege Dar Es Salaam. Himid Mao baada ya kuwasili Nahodha wa Kilimanjaro Stars John Bocco baada ya kutua Dar akielekea katika basi. John Bocco na kocha mkuu na msaidizi wake wakizungumza jambo Shomari Kapombe ndani ya basi la timu ya Taifa Hassan Kessy akipanda basi la Stars Mshauri wa Kilimanjaro Stars na kocha wa Taifa Stars Charles Boniface Mkwasa aki...