Skip to main content

Posts

TAZAMA PICHA PAMOJA NA MATUKIO YOTE YA MSIBA WA DR. SENGONDO MVUNGI JIJINI DAR LEO

Jeneza lenye mwili wa marehemu  Dkt.Sengondo Mvungi, likiwasili kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam,leo kwa ajili ya kuagwa  Jeneza likipelekwa sehemu iliyoandaliwa  Mashada ya maua na picha ya marehemu   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,  akizungumza kutoka salamu za rambi rambi za serikali wakati wa shughuli za kuaga mwili wa marehemu,  Dkt.Sengondo Mvungi,kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam,leo. Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Katiba Jaji Joseph Sinde Warionba akiongea machache wakati wa shughuli za kuaga mwili wa marehemu,  Dkt.Sengondo Mvungi,kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam,leo.  Makamu wa Rais Dkt Gahlib Bilali, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Katiba Jaji Joseph Warioba, Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Mhe Angela ...

Rais Dk.Shein azungumza na Uongozi wa Wizara Habari

Baadhi ya Viongozi mbali mbali wa  Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo,wakiwa,katika mkutano wa utekelezaji wa Mpango wa kazi za Wizara hiyo,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,katika  Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar. [Picha na Ramadhan Othman Ikulu.] Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(kulia) akisikiliza taarifa ya utekezaji wa kazi za Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo, iliyosomwa na Waziri Said Ali Mbarouk,(kushoto)  katika mpangilio wake wa kuzungumza na kila Wizara katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar,(katikati) Katibu Mkuu Kiongozi Dk.Abdulhamid Yahaya Mzee.[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.] Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo, katika utekelezaji wa Mpango wa kazi za Wizara hiyo,katika  Ukumbi wa ...

KIUNGO MATATA STEVEN MAZANDA: MAANDALIZI YA MAPEMA YAMETUPA MAFANIKIO, NAPENDA VIJANA WANAVYOCHEZA SOKA KWA SASA!!

Kiungo jembe wa Mbeya City FC, Steven Mazanda (waliosimama, wapili kulia) amesema hawana presha na kasi ya timu pinzani, mzunguko wa pili wako fiti balaa! Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam Kiungo wa Mbeya City, Steven Mazanda, amesema siri ya mafanikio ya kikosi chao katika mzunguko wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara uliomalizika novemba 7 mwa huu na klabu hiyo kumaliza katika nafasi ya tatu kwa pointi 27 sawa na Azam fc katika nafasi ya pili ni maandalizi ya mapema waliyofanya pamoja na nidhamu kubwa ya wachezaji kuanzia uwanjani na nje ya uwanja. “Unajua sisi tulijiandaa mapema sana, na ndio maana unaona kikosi kinacheza kitimu na kila mtu anavutiwa. Kiukweli kumekuwepo na changamoto za ushindani, lakini tunaingia katka kila mechi kuhitaji ushindi”. Alisema Mazanda. Mazanda ambaye  amewahi kuzichezea timu za Tukuyu, Simba, Mtibwa na Kagera Sugar, kabla ya kuisaidia Mbeya City kupanda daraja ameongeza kuwa mzunguko wa pili hakika utaku...

VIJANA MKOANI KILIMANJARO WAHIMIZWA UTEKELEZAJI WA MALENGO YA MILENIA

Afisa Habari wa Kituo cha Umoja Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma Ledama akizungmza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Umbwe mkoani Kilimanjaro juu ya umuhimu wa kujihusisha na kazi za Umoja wa Mataifa wakati wa ziara za kutembelea shule mbalimbali za mkoa huo. Na. Mwandishi wetu. Vijana wa shule za sekondari nchini wameaswa kuwa mabalozi wazuri pindi watakapomaliza masomo yao juu ya kuhamasisha utekelezaji wa malengo ya milenia kwa sababu ni dira ya maendelo ya taifa na dunia kwa ujumla. Akizungumza na wanafunzi wa shule ya Wasichana Kibosho, Lyamungo na Umbwe sekondari hivi karibuni, Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, Bi. Usia Nkhoma Ledama amesema malengo ya milenia yanagusa Nyanja zote za maendelo kwa vijana walio na wasio mashuleni. Bi. Nkhoma amewataka wanafunzi wafanye kazi za kujitolea na kuhakikisha wanapeleka elimu waliopata kupitia vilabu vya Umoja wa Mataifa kwa jamii na kuhamasisha dhana ya kujitolea kwa maslahi ya nchi. “kila nda...

MZIZIMA ROTARY CLUB YAMPA TUZO MKURUGENZI WA SHIRIKA LA NYUMBA (NHC)KWA UTENDAJI ULIOTUKUKA

Rais wa Mzizima Rotary Club Bw. Ambrose Ntageki Nshala akikabidhi cheti maalum cha kutambua utendakazi na mchango wa Nehemia Mchechu Kyando Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba (NHC) wakati Club hiyo ilipomkabidhi cheti na tuzo maalum katika hafla iliyofanyika kwenye hoteli ya Courtyard Upanga jijini Dar es salaam. Rais wa Mzizima Rotary Club Bw. Ambrose Ntageki Nshala akikabidhi tuzo  maalum ya kutambua utendakazi na mchango wa Nehemia Mchechu Kyando Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba (NHC) wakati Club hiyo ilipomkabidhi cheti na tuzo maalum katika hafla iliyofanyika kwenye hoteli ya Courtyard Upanga jijini Dar es salaam. Kushoto ni Paul Mashauri na na wajumbe wengine wa Rotary Club wakimpigia makofi Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba NHC Bw. Nehemia Kyando hayupo pichani mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba NHC Bw. Nehemia Kyando akitoa shukurani zake kwa Rais wa Rotary Club na wajumbe wake mara baada ya kukabidhiwa tuzio hiyo. kulia ni...

Kizungumkuti cha amani kati ya M23 na DRC

  DRC ilisusuia shughuli ya kutia saini mkataba wa amani kutokana na maandiko yake Shughuli ya kutia saini mkataba wa amani kati ya waasi wa M23 na serikali na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo,iliyokukuwa imepangwa kufanyika Jumatatu , iligonga mwamba. Hii ni kutokana na serikali ya Congo kusema kuwa mkataba huo uangaliwe upya na hivyo kulazimisha shughuli hiyo kuahirishwa. Mpatanishi wa pande hizo mbili Ofuono Opondo wa Uganda, alisema kuwa pande hizo hazikuwa tayari kuonana ana kwa ana baada ya DRC kusema kuwa M23 watie saini mkataba katika chumba tofauti na kisha wapewe wao kuusaini. Hata hivyo mpatanishi alisema haiwezekeni kwa hilo kufanyika kwa sababu pande zinazozozana lazima zikae katika chumba kimoja kwa ajili ya kufanikisha juhudi za upatanishi. Kundi la waasi la M23 lilisitisha uasi wao baada ya kupata kipigo kutoka kwa wanajeshi wa DRC wakisaidiwa na wanajeshi wa Umoja wa Mataifa waliowafurusha kutoka maficho yao ya milimani katika mpaka w...

BAJETI YA SERIKALI YA MWAKA 2014 IPUNGUZE VIFO VYA WAJAWAZITO

ZAIDI ya Wanawake 8,700 hufariki duni kila mwaka nchini Tanzania kutokana na matatizo ya ujauzito na hasa wakati wa kujifungua. Takwimu hizi zinaonesha takribani wanawake 24 hupoteza maisha kila siku huku ikikadiriwa mmoja kufa kila baada ya saa moja. Hata hivyo wataalamu wa afya wanasema moja kati ya sababu zinazochangia vifo hivi  ni kukosekana kwa huduma za dharura katika Vituo vya Afya wakati wa kujifungua. Hata hivyo Serikali ya Tanzania mwaka uliopita katika ahadi zake imeahidi kupunguza vifo hivi kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2015. “Si sahihi mama mjamzito kufa wakati wa kujifungua au si sahihi mama huyu kupoteza uhai wake kwa kuugawa kwa kiumbe anachokileta duniani, hii haiwezi kukubalika. Na inasikitisha zaidi pale maisha ya mama huyu yanapotea hata kwa mambo ambayo yanaweza kuzuilika,” anasema Rais Kikwete katika hotuba yake mbele ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ( U.N) Ban Ki-moon. Wewe pia unaweza kushiriki katika kupigania kutokomeza ...