Skip to main content

Majambazi wavamia kituo kikuu cha Polisi Mwanza




 
Wizi huo wa ajabu ulitokea Julai 18, mwaka huu, ambapo majambazi hao walivunja kituo hicho ambacho ndani yake kuna Ofisi ya Mkuu wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC).

Mwanza. Majambazi wamevunja ofisi za Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Mwanza na kuiba mali mbalimbali vikiwemo vielelezo vya watuhumiwa walio na kesi mahakamani.


Wizi huo wa ajabu ulitokea Julai 18, mwaka huu, ambapo majambazi hao walivunja kituo hicho ambacho ndani yake kuna ..........
Ofisi ya Mkuu wa Polisi Mkoa wa Mwanza (RPC).
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zilibaini kuwa majambazi hao walivunja ghala la vielelezo vya washtakiwa, chumba cha ghala la vipuri vya magari ya polisi, zikiwemo ofisi za Wapelelezi wa Makosa ya Jinai na Waendesha Mashtaka.
Majambazi hao wanadaiwa kuiba majalada ya kesi, begi lililokuwa na vielelezo vya washtakiwa, kompyuta ndogo mbili (Laptop) za ushahidi na kutoweka.
Wizi huo uliotokea usiku na kubainika asubuhi, ambapo watu hao ambao idadi yao haijajulikana wanadaiwa waliweza kufanikiwa kuingia ndani ya ofisi hizo za polisi, kwa kuvunja madirisha mawili ya chumba cha ghala la ofisi za Mkaguzi wa Elimu Kanda ya Ziwa ambazo zinapakana na Kituo Kikuu cha Polisi cha Kati cha Jijini Mwanza, kisha kufanikisha wizi huo.
Habari zilizopatikana kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zinaeleza kwamba wizo huo ambao ulilenga ofisi ya vielelezo na mashtaka, ulipangwa kwa umakini na kutekelezwa bila ya polisi waliokuwa zamu usiku huo kubaini lolote.
Kwa mujibu wa maelezo wezi hao inadhaniwa ni watu wenye uzoefu na jengo hilo, wakiwa na nia ya kuchukua vielelezo mbalimbali pamoja na mafaili muhimu ya kesi kubwa.
Hili ni tukio lingine kubwa kutokea kwa Jeshi la polisi Mkoa wa Mwanza sambamba na tukio la kuuawa kwa aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, Oktoba 13, mwaka jana ambaye alipigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi saa nane usiku wakati akitoka katika kikao cha harusi.
Kauli ya Kamanda Mangu:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Evarist Mangu, amethibitisha kutokea kwa wizi huo na kusema jeshi lake linafanya uchunguzi wa kina kubaini waliohusika, na kusisitiza kuwa kama ni askari wake ama watu toka nje hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
Alisema wezi hao waliingilia katika ofisi ya Ukaguzi Elimu Kanda ya Ziwa ambako walivunja madirisha mawili, moja likiwa ni kuingia ndani ya ghala la ofisi za elimu na dirisha lingine la kutokea nje ya ghala hilo, kisha kuvunja dirisha la ndani ya majengo ya polisi na kufanikisha wizi huo.
“Wezi hao walipiga jeki nondo za madirisha hayo, hivyo kung’oka na kuingia ndani kisha kwetu, walianza kuingia katika ghala la polisi la kuhifadhia vifaa vya ofisi vya Jeshi la polisi, lakini inaonekana walikosa cha kuiba, huko walipanda darini na kutokea katika chumba kingine nako hawakuiba, lakini katika chumba cha vielelezo ambako walikuta begi lililokuwa na nguo za vielelezo pamoja na kompyuta ndogo mbili, Lap Top, ambazo walitoweka nazo,” alieleza Kamanda Mangu

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...