Skip to main content

Posts

Showing posts from December 13, 2015

soma Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi yaa Disemba 19

Waziri wa Mambo ya Nje Dk Mahiga Kuzungumza Na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Kuhusu Hali Ya Usalama Nchini Burundi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga atafanya ziara ya..............

Kasi ya Rais Magufuli Yabaini Vyeti FEKI 219.......Waziri Ataka Hatua Kali za Kisheria Zichukuliwe Dhidi Yao

Kasi ya Mawaziri  wa Rais John Pombe Magufuli kufanya ziara za kushtukiza na kutoa maagizo kwa watendaji imeanza kufumua uozo baada ya jana kubainika kuwa watumishi 219 kati ya 704  wa serikali wameajiriwa kwa..............

Kauli Ya Mwenyekiti Freeman Mbowe Kuhusu Uamuzi Wa Bodi Ya MCC Kuzuia Msaada Wake Wa Trilioni 1 Kwa Serikali Ya Tanzania

Muda mfupi baada ya Bodi ya MCC kutoa taarifa inayoonesha Tanzania haitapata msaada kutoka shirika hilo kama ilivyotarajiwa kwa ajili ya...........

Profesa Muhongo Kafuta Likizo Zote Za Wafanyakazi wa Tanesco.......Kawaagiza Pia Washushe Bei ya Umeme

Bei ya umeme inatarajia kushuka wakati wowote kuanzia sasa baada ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (pichani )kuliagiza Shirika la Umeme (Tanesco), kushusha..........

Watumishi 10 Tanesco Wasimamishwa Kazi Kwa Upotevu wa Milioni 100

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme (Tanesco), Felchesmi Mramba, amewasimamisha kazi maofisa 10 wakiwamo.........

TCRA Yatoa miezi Sita hadi June 16, 2016 kuzifunga simu zote feki Tanzania.....Hakiki Simu Yako Mapema

UTANGULIZI: Vifaa vya mawasiliano vya mkononi – hususan simu za kiganjani na vifaa vya mawasiliano vya kiganjani (tablets) – vina namba maalum inayovitambulisha. Namba hiyo inajulikana kama................

Wanyarwanda Wengi Waunga Mkono Mabadiliko ya Katiba Kumruhusu Paul Kagame Kuendelea Kutawala

Wanyarwanda wameunga mkono kwa wingi marekebisho ya katiba ambayo yatamruhusu Rais Paul Kagame kuendelea kuongoza, matokeo ya awali ya..............

Taasisi 1,200 Duniani Zampa Tuzo ya Amani Edward Lowassa

Taasisi 1,200 duniani zitampa aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa Tuzo ya.........

TAZAMA PICHA NA CHANZO kwenye ajali ya basi la abiria na lori lililotokea Iringa

Kwenye taarifa ambazo zimenifikia muda mfupi uliopita iko pia inayohusu ajali iliyotokea leo December 18 2015 maeneo ya Kilolo Iringa… Kwenye ajali hiyo Jeshi la Polisi limethibitisha kuwa watu 12 wamefariki na wengine 18 kujeruhiwa, mazingira ya ajali yanaonesha lori la mizigo lilipoteza mwelekeo na kuligonga basi hilo.

TAZAMA VIDEO MPYAAAAA YA Izzo Bizness ft Mwana FA & G-Nako - Shem Lake (Official Music Video)

TAZAMA JINSI Dk.Mwaka ALIVYO MKIMBIA Mh. Kigwangallah alivyofanya ziara ya kustukiza ForePlan clinic

Jose Mourinho afutwa kazi Chelsea

Meneja wa klabu ya Chelsea ya Uingereza amefutwa kazi baada ya..........

TAZAMA PICHA ZA MATUKIO YOTE YA JINSI MWANDISHI WA HABARI DOTTO MNZAVA ALIVYOZIKWA HUKO VUDEE SAME MKOANI KILIMANJARO

Magufuli amfuta mkuu wa kupambana na rushwa

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Dkt Edward Hoseah, na pia....

TAFFA Yaibua Mapya Ya Utoroshaji Wa Kontena Bandarini

CHAMA cha Mawakala wa Forodha nchini (TAFFA) kimesema kuwa wizi wa kontena bandari ya Dar es Salaam na kusababisha serikali kukosa mapato ni tatizo la muda mrefu ambalo ni limekuwa likisababishwa na watumishi wa bandari.   Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Rais wa TAFFA, Steven Ngatunga alisema tatizo lilojitokeza ya uondoshaji wa...........

Uturuki Kuisaidia Tanzania Kufanikisha Mpango wa Elimu Bure

Serikali ya Uturuki imeahidi kuisaidia  Serikali ya Tanzania kufanikisha mpango wa utoaji wa elimu bure kwa wanafunzi utakaoanza January mwakani. Hayo yalizungumzwa jana na Balozi wa Uturuki nchini Bi Yasemin Eralp  alipokuwa akizungumza na..........

Simbachawene Aagiza Taka Zilizokusanywa Wakati Wa Uhuru Disemba 9 Zizolewe Kabla Ya Disemba 20

WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi,Utumishi na Utawala bora George Simbachawene amewaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurungenzi wote wa halmashari nchini kuhakikisha wanazoa taka zote zilizokusanywa wakati wa ..........

Washitakiwa Watatu wa TRA Wanaohusika na Utoroshaji Makontena Wapewa Dhamana.......Yupo Masamaki na Wenzake Wawili

Mahakama kuu ya Tanzania imeridhia dhamana kwa washitakiwa watatu wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA wanaokabiliwa na mashitaka ya kutoa makontena 329 bandarini bila............

Mbowe Azungumzia Kasi ya Rais Magufuli.....Adai Kuwa Mpinzani Haimaanishi Upinge Kila Kitu

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amezungumzia kasi aliyoanza nayo rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli pamoja na baraza lake la mawaziri. Akizungumza jana na mwandishi wa habari wa Azam TV, Mbowe alisema kuwa rais Magufuli ameanza vizuri kiutendaji na kwamba ameanza kuzifanyia kazi hoja zilizokuwa zikihubiriwa na Chadema ndani na nje ya Bunge. “Hoja ya kubana matumizi ya serikali, hoja ya kupunguza sherehe za kitaifa, hoja ya kupunguza safari za nchi za nje kwa viongozi wetu, hoja ya kupunguza watumishi wa umma ambao hawana umuhimu, hoja ya kuwa na serikali ndogo. Haya mambo tulizungumza siku zote na hawa hawa wa Chama cha Mapinduzi ndio waliokuwa wanayapinga haya,” alisema Mbowe. Mbowe alieleza kuwa dhana ya upinzani sio kupinga kila kitu kinachofanywa na serikali hivyo chama chake hakitakuwa tayari kupinga mambo mema yanayofanywa na serikali ya awamu ya tano kama baadhi ya watu wanavyotarajia, bali kitajikita katika kujadili na kuibua hoja za

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Disemba 16

Chama cha Wahasibu Tanzania (TAA) Chaahidi Kupambana Na Wahasibu Wala Rushwa, Wezi na Mafisadi

CHAMA cha Wahasibu Tanzania (TAA) kimetishia kuwaondoa wahasibu waliokuwepo kwenye daftari la chama hiko endapo watakiuka taratibu na maadili ya kazi kulingana na matakwa ya chama hicho ikiwemo ya rushwa, wizi na ufisadi. Hayo yalisemwa jana  jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa chama hicho, Fred Msemwa katika mazungumzo yake na wanahabari wakati akitoa pongezi na kuunga mkono kwa jitihada za serikali ya awamu ya nne juu ya ukusanyaji wa mapato. Msemwa alisema kuwa wahasibu na wakaguzi wa hesabu, wanatakiwa kufanya kazi kwa mujibu wa taaluma zao kwa kufuata miongozo ya sheria Na.33 ya 1973 inayosimamia taaluma ya uhasibu na ukaguzi wa hesabu Tanzania. Amesema kuwa chama hicho hakitasita kumundoa mhasibu yoyote atakayeshiriki katika wizi na mambo mengine kinyume na matarajio ya wananchi ataondolewa haraka.

Mapigano ya Wafugaji na Wakulima Morogoro: Serikali Yabomoa Mabanda ya Wafugaji Na Kupiga Mnada Ng'ombe Zao

WAFUGAJI waliovamia maeneo ya wakulima katika kijiji cha Dihinda wilayani Mvomero mkoani Mogorogo na kusababisha mapigano yaliyoua mkulima na ng’ombe 71, wamekimbia kijijini hapo na kutokomea kusikojulikana. Akizungumzia hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Wilaya ya Mvomero, Mkuu wa Wilaya hiyo, Betty Mkwasa alisema ulinzi bado umeimarishwa eneo hilo, na kwamba wafugaji waliovamia wamekimbia. “Wafugaji wamekimbia na sisi tutateketeza maboma yao, kwa sababu walivamia eneo hili la wakulima na ng’ombe walioachwa wamepigwa mnada na fedha imeingizwa kwenye mfuko wa serikali ya kijiji hicho,” alisema Mkwasa. Aidha, katika msako uliofanywa kwa ushirikiano wa Serikali ya Wilaya na Polisi silaha moja ya askari iliyochukuliwa ilipatikana na kwamba wakulima wametolewa hofu na kusisitizwa kuendelea na kazi zao kama kawaida. Alifafanua kwamba hali kwa sasa kijijini hapo ni shwari na kwamba mifugo iliyouawa kwa kukatwakatwa mapanga yote imeshafukiwa na uongozi wa seri

Mchungaji na Mkewe Watiwa Mbaroni kwa Kumfungia Ndani Mtoto Wao Mlemavu kwa Miaka 12

POLISI mkoani Singida inamshikilia Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste Itaja na mkewe kwa tuhuma za kumfungia ndani ya chumba mtoto wao mlemavu wa viungo kwa miaka 12 bila kutoka nje. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni David Mtipa (59) ambaye ni Mchungaji wa Kanisa hilo na mkewe Mariam Philipo (45) wote wakazi wa kijiji cha Itaja katika tarafa ya Mgori wilayani Singida. Kamanda Sedoyeka alisema tukio hilo liligundulika juzi katika kijiji hicho baada ya Polisi kupata taarifa za siri kutoka kwa wasamaria.     Akielezea tukio hilo, Kamanda Sedoyeka alisema watuhumiwa walimfungia ndani ya chumba mtoto huyo, Timotheo David (30) kwa muda wa miaka 12 huku huduma zote za kibinadamu, ikiwemo haja ndogo na kubwa pamoja na chakula zikifanyika humo ndani. “Baada ya timu ya askari wa Upelelezi na Ofisa Ustawi wa Jamii kufika eneo hilo wakiwa na viongozi wa kijiji na kufanya mahojiano, watuhumiwa walikiri kumfungia chumbani mtoto wao huy

Lowassa kuzunguka nchi nzima kuanzia kesho

Aliyekuwa mgombea urais wa Chadema akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa ataanza ziara ya kuzunguka nchi nzima kuwashukuru Watanzania kwa kumpigia kura katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 na kesho atakuwa Tanga. Katika ziara hiyo, Lowassa ataambatana na viongozi waandamizi wa Chadema na Ukawa kuwashukuru wananchi kwa namna walivyounga mkono upinzani na ajenda nzima ya mabadiliko katika Uchaguzi Mkuu uliopita. Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene imesema kiongozi huyo atatoa shukrani zake kwa wananchi kwa jinsi wanavyoendelea kuweka matumaini yao kwa upinzani. Taarifa hiyo ilieleza kwamba wananchi bado wanaamini kwamba upinzani ndiyo nguzo imara wanayoitegemea katika kuwaletea mabadiliko ya kweli kwa ajili ya maendeleo yao na ustawi wa Taifa kwa ujumla. “Wananchi wanastahili shukrani kwa imani hiyo kubwa ambayo ni ishara ya wazi kuwa matumain

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu Afanya Ziara ya Kushtukiza Hospitali ya Muhimbili Leo na Kukuta Mashine za CT Scan na MRI Zimeharibika Tena

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Ummy Mwalimu amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo na kukuta mashine za CT Scan na MRI hazifanyi kazi. Katika ziara hiyo aliyoifanya asubuhi ya leo, alikutana na mzee wa miaka 90 ambaye alikuwa akisubiri huduma hiyo tangu jana. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Wa Hospitali hiyo, Lawrence Museru, mashine hizo ziliharibika tangu juzi na hivyo huduma zilisimama tangu jana asubuhi. Tatizo kubwa katika machine ya CT Scan picha hazisomeki vizuri na MRI imeharibika spea ambazo kwa mujibu wa uongozi wa hospitali hiyo, matengenezo yanaanza leo. Hata hivyo, Mwalimu ameagiza uongozi wa hospitali hiyo ya rufaa kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha kuwa mashine hizi zinarudi katika hali yake ya kawaida. Mashine hizo zimeendelea kuwa changamoto kwa hospitali hiyo licha ya Rais John Magufuli kufanya ziara ya kushtukiza na kukuta hali kama ya leo.

Tazama video ya Mwana FA akiweka wazi walivyopatana na Hammy B na kuitambulisha Asanteni kwa Kuja

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Disemba15