Skip to main content

Mapigano ya Wafugaji na Wakulima Morogoro: Serikali Yabomoa Mabanda ya Wafugaji Na Kupiga Mnada Ng'ombe Zao


WAFUGAJI waliovamia maeneo ya wakulima katika kijiji cha Dihinda wilayani Mvomero mkoani Mogorogo na kusababisha mapigano yaliyoua mkulima na ng’ombe 71, wamekimbia kijijini hapo na kutokomea kusikojulikana.

Akizungumzia hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Wilaya ya Mvomero, Mkuu wa Wilaya hiyo, Betty Mkwasa alisema ulinzi bado umeimarishwa eneo hilo, na kwamba wafugaji waliovamia wamekimbia.

“Wafugaji wamekimbia na sisi tutateketeza maboma yao, kwa sababu walivamia eneo hili la wakulima na ng’ombe walioachwa wamepigwa mnada na fedha imeingizwa kwenye mfuko wa serikali ya kijiji hicho,”alisema Mkwasa.

Aidha, katika msako uliofanywa kwa ushirikiano wa Serikali ya Wilaya na Polisi silaha moja ya askari iliyochukuliwa ilipatikana na kwamba wakulima wametolewa hofu na kusisitizwa kuendelea na kazi zao kama kawaida.

Alifafanua kwamba hali kwa sasa kijijini hapo ni shwari na kwamba mifugo iliyouawa kwa kukatwakatwa mapanga yote imeshafukiwa na uongozi wa serikali ya wilaya umepanga kuingia mkataba na viongozi wa vijiji na kata ili kudhibiti, migororo baina ya makundi hayo.

Alisema katika kudhibiti matukio ya mapigano au uvunjifu wa sheria na mpango wa matumizi bora ya ardhi, Mvomero itaanza kuingia mkataba na watendaji wa vijiji na kata na iwapo migogoro itatokea, wao ndio watawajibishwa.

Awali Desemba 12, mwaka huu, kundi la wafugaji wa jamii ya Kibarbaig waliwavamia wakulima na kuanza kuwashambulia kutokana na mmoja wa wafugaji ambaye mifugo yake iliharibu mazao ya mkulima kutakiwa kulipa fidia ya Sh 200,000.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...