Skip to main content

Posts

Showing posts from December 1, 2013

FAHAMU KUHUSU UNDANI WA KIFO CHA MANDELA

SIYO habari tena, kwani dunia nzima inajua kuhusu kifo cha shujaa wa Afrika, nembo ya mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi, komredi aliyefungwa jela miaka 27 akitetea usawa baina ya wananchi wa Afrika Kusini, Nelson Rolihlahla Mandela. Risasi Jumamosi, kwa msaada wa vyanzo mbalimbali, linamulika kwa undani chanzo hasa cha kifo cha Mandela, aliyefikwa na mauti usiku wa kuamkia jana, Desemba 5, mwaka huu akiwa na umri wa miaka 95. Mandela akiwa na mkewe Graca Machel ( kushoto ) na mtalaka wake, Winnie Mandela ( kulia ). Ripoti za ndani zaidi, zinabainisha kuwa afya ya Mandela ilianza kuleta mushikeli tangu akiwa kijana na kwa mantiki hiyo, sehemu kubwa ya maisha yake alisumbuliwa na maradhi. UNDANI WA MARADHI YALIYOMUUA Ripoti za wataalamu mbalimbali kuhusu afya ya Mandela, kwa pamoja zinatoa majibu kwamba chanzo cha maradhi ya mapafu ambayo ndiyo hasa yaliyokatisha uhai wake ni matokeo ya ukatili aliokuwa anafanyiwa gerezani, kipindi akiwa mfungwa wa kisiasa. Habari zinase

FAMILIA YA MWINYI YAZUA TAFRANI

Hii ndo nyumba yenyewe juzikati ilizua tafrani mtaani kufuatia mzozo mkubwa wa nyumba kati ya mjukuu wa Mzee Mwinyi, Abdi Hassan Mwinyi na anayedai ni mmiliki wa kurithi, Edward Francis Bogwe. Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita, Mwananyamala-Komakoma, Dar ambapo mtoto wa rais mstaafu huyo aitwaye Abas Mwinyi aliongoza sekeseke mtaani. Mtoto wa Mwinyi ( wa pili kutoka kushoto), Abas akiwa nyumbani hapo. Ishu ilikuwa hivi; miezi kadhaa iliyopita, Edward alimfikisha Mahakama ya Ardhi chini ya Jaji Kombolwa, Abdi akimtaka ahame kwenye nyumba hiyo ambayo ni mali ya familia, aliachiwa na marehemu baba yake, Francis Bogwe. Baada ya kusikiliza utetezi wa pande zote mbili, mahakama ikaamuru Abdi ahame kwenye nyumba hiyo kwa vile ni mali ya Francis. Francis akiongozana na madalali alikwenda kumtoa Abdi na vitu vyake, ikiwemo familia na kupiga kufuli milango muhimu ya kuingilia ndani na kuondoka nyumba ikiwa tupu. Lakini siku mbili mbele, Abas akiwa na ndugu zake weng

WATANZANIA WAASWA KUHESHIMU HAKI ZA MTOTO

Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Tanzania (THBUB), Jaji Mstaafu Amir Manento akizungumza na waandishi wa habari wakati mdahalo wa Siku ya Kimataifa ya Haki za Binadamu kuelekea maadhimisho ya siku hiyo ambayo hufanyika tarehe 10 mwezi Disemba kila mwaka. .Jaji Manento asema ni uvunjifu wa sheria kwenda na watoto harusini Na Damas Makangale, MOblog WAZAZI na Walezi wameaswa kuacha mara moja tabia ya kwenda na watoto katika sherehe na harusi mbalimbali za kwa sababu ni kosa la Jinai kwa mujibu wa sheria na Haki za Mtoto. MOblog inaripoti. Akizungumza kwenye mdahalo wa Siku ya Kimataifa ya Haki za Binadamu ambao huadhimisha kila tarehe 10 mwezi Disemba kila mwaka, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Tanzania, Jaji Mstaafu Amir Manento amesema kwa mujibu wa sheria na Haki za Mtoto wazazi au walezi hawaruhusi kwenda na watoto katika sherehe za usiku. “wazazi na walezi na watu wa kawaida wanamazoea ya kwenda na watoto kwenye s

WAZIRI MKUU MHE. PINDA AKAGUA MAJI YENYE SUMU TOKA VIWANDANI MOROGORO

Maji yenye sumu, kemikali na tindikali kutoka kwenye viwanda vya 21st Century cha nguo, Morogoro Canvanse na kiwanda cha Magunia Morogoro yakitiririka kuelekea mtoni baada ya viwanda hivyo kushindwa kuzingatia masharti ya kusafisha maji hayo kabla ya kuyaelekeza  mtoni. Mheshimiwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda alitembelea eneo hilo Desemba 7, 2013.(Picha na Ofisi aWaziri Mkuu) Waziri Mkuu, MIzengo Pinda , Viongozi wa Baraza la Mazingiea nchini, NEMC na viongozi wa mkoa wa Morogoro wakitazama maji yenye sumu, kemikali na tindikali yaliyoekekezwa mtoni yakitoka kwenye viwanda vya 21st  Century cha nguo, Morogoro  Canvanse na kiwanda cha magunia cha Morogoro wakati alipotembela eneo Kihonda mbuyuni kukagua  athari za maji hayo.(Picha na  Ofisi ya Waziri Mkuu)

VIJANA WA TANZANIA REDCROSS(TRCS) WALIOFUZU MAFUNZO YAO HIVI KARIBUNI WAANZA KUTOA ELIMU KWA JAMII JIJINI DAR-ES-SALAAM

Kijana wa pili kutoka kulia ni Samson kutoka Mzizima branch akiongoza jopo la wanafunxi wenzie aliofuzu nao. Vijana wa Redcross Tanzania waliofuzu mafunzo ya kutoa elimu katika jamii,wakiwa katika picha ya pamoja na Miss Maria from Crescent Societies wa pili kutoka kushoto. Wazee wa wilaya ya Kinondoni wakipoa habari njema kutoka kwa vijana wa Redcross Tanzania

KINANA AZUNGUMZA NA WANAFUZNI WA ELIMU YA JUU NJOMBE, ASHIRIKI UZINDUZI WA ALBAM YA “AMANI TANZANIA”

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wanafuzni wa vyuo vikuu mkoani Njombe wakati alipowasili katika Chuo cha maendeleo ya jamii Njombe ambapo amekutana na wanafunzi mbalimbali wa elimu ya juu mkoani humo na kusikiliza kero zao mbalimbali Kinana amefanya ziara maalum ya kikazo katika koa wa Njombe baada ya kumaliza ziara yake ndefu ya mikoa ya Ruvuma kamati  na Mbeya Alhamisi iliyopita akiongozana na wajumbe wa kamati kuu ya CCM Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi, kinana pia alishiriki katika uzinduzi wa albam ya kikundi cha sanaa cha Vicheko Sanaa Group cha Njombe uliofanyika mjini Njombe leo (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-NJOMBE) Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa akisalimiana na Mhadhili wa Chuo cha Amani Njombe wakati alipowasili katika mkutano na wanafunzi wa elimu ya juu mjini Njombe. Baadhi ya wanafunzi wakiwa katika

HIVI NDIVYO WATANZANIA WANAVYOMUENZI NELSON MANDELA

Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela Rais Jakaya Kikwete wa nchi hiyo pia ameagiza kuwa katika kipindi hicho cha siku tatu bendera zote zitapepea nusu mlingoti. Kufuatia kifo hicho Rais Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini na kupitia kwake kwa mkewe Bi Graca Machel, wanafamilia wote na wananchi wote wa Afrika ya Kusini kufuatia kifo cha Mzee Nelson Mandela kilichotokea tarehe 5 Desemba, 2013 baada ya kuugua kwa muda mrefu. Rais ameuelezea msiba huu kuwa ni msiba mkubwa kwetu sote. "Afrika ya Kusini, Afrika na dunia kwa ujumla imepoteza mtu mashuhuri na shujaa mkubwa wa Karne ya 20 na 21.Tunaelewa machungu waliyonayo wananchi wa Afrika ya Kusini kwa kupoteza kiongozi shupavu, jasiri, mwana mapinduzi , mvumilivu na mstahimilivu". Ameongeza Rais Kikwete. Rais amemuelezea Mzee Mandela kuwa ni kielelezo cha aina yake kwa wanada

CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAKABIDHI TREKTA KWA VIJANA WA NJOMBE WANAOJISHUGHULISHA NA KILIMO

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi funguo za Trekta kwa Mwenyekiti kwa vijana Tumsume Shemgogo lililotolewa na chama cha Mapunduzi CCM  kwa vijana wa mkoa wa Njombe katika makabidhiano yaloyofanyika kwenye Kambi ya vijana iliyopo kwenye kijiji cha Mlengu Kata ya Kiangala Tarafa ya Ikuo mkoani Njombe ambapo kambi hiyo ina eneo lenye ukubwa wa  hekta 300 za mashamba, Kinana aliahidi kutoa  trekta hilo wakati alipofanya ziara ya kikazi mkoani Njombe mwezi Agosti mwaka huu  baada ya kuelezwa jinsi vijana hao walivyojiunga pamoja katika kikundi na kuamua kushughulika na kilimo ili kujkwamua kiuchumi, Leo Abdulrahman Kinana alishiriki kulima kwa trekta kabla ya kukabidhi trekta hilo kama anavyoonekana katika baadhi ya picha akilima shambani  kwa trekta.  Kushoto anayeshuhudia makabidhiano hayo ni Nape Nnauye Katibu wa NEC  Siasa, Itikadi na Uenezi, Katika Ziara hiyo Kinana  pia ameongozana  na Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na