Skip to main content

Posts

Showing posts from July 6, 2014

Al-Shabaab washambulia ikulu Somalia

Ikulu ya Rais iliwahi pia kushambuliwa mwezi Februari Vikosi vya serikali Somalia vimefanikiwa kuidhibiti upya ikulu ya rais katika mji mkuu Mogadishu baada ya wapiganaji wa Al Shabaab kuishambulia. Maafisa wanasema washambuliaji wapatao watano kutoka kundi la al-Shabab - waliuawa walipoingia katika eneo la ikulu hiyo. Taarifa zinazohusiana Somalia Washambuliaji hao wanadaiwa kulipua bomu lililotegwa kwenye gari karibu na langu kuu la Ikulu hiyo. Waziri wa habari wa Somalia Mustaf Dhuhulow Waziri wa habari na mawasiliano wa Somalia Mustaf Dhuhulow ameambia BBC kuwa tayari mmoja wa washambuliaji hao amekamatwa na anahojiwa na polisi. Waziri Mustaf amesema, '' Walishambulia ikulu

BRAZIL WAWEKA BONGE LA REKODI…HAIJAWAHI KUTOKEA TANGU KOMBE LA DUNIA KUANZA 1930, YACHAPWA NYUMBANI 7-1 NA UJERUMANI

Ujerumani wameipiga Brazil kipigo cha mbwa mwizi. Na Baraka Mpenja KWA Muda mrefu wananchi wa Brazil waliandamana wakipinga nchi yao kuandaa fainali za kombe la dunia kwasababu kiasi kikubwa cha fedha kimetengwa. Walikuwa wakihuzunishwa na matumizi makubwa ya fedha kwa ajili ya kuandaa miundo mbinu ya kombe la dunia, wakati maisha yao yakiwa katika hali mbaya. Huduma mbovu za jamii, umasikini wao uliwahamasisha kuandamana na kuleta sintofahamu ya kisiasa. Brazil walienda kwa kujivuta na mnamo juni 12 mwaka huu wakasahau shida zote na kushuhudia timu yao ya Taifa ikicheza mchezo wa ufunguzi dhidi ya Croatia. Walipata ushindi wa mabao 3-1 na kufurahia matokeo hayo. Faraja pekee kwa wananchi maskini wa Brazil ilikuwa ni kuona timu yao inafanya vizuri na kubeba kombe. Walikuwa wanafurika uwanjani, kwenye kumbi za kuoneshea mpira, lengo ni kutaka kuona timu yao inafanya nini. Hawaamini: Fernandinho, Maic

MIROSLAV KLOSE AVUNJA REKODI NA KUWA MFALME WA MABAO KOMBE LA DUNIA, AMTINDUA GWIJI WA BRAZIL RONALDO

Mvunja rekodi: Miroslav Klose ni mfungaji bora katika historia ya kombe la dunia. Miroslav Klose amevunja rekodi ya Ronaldo na kuwa mfungaji mwenye mabao mengi zaidi katika historia ya fainali za kombe la dunia. Mshambuliaji huyo wa Ujerumani alifunga bao la pili katika ushindi wa mabao 7-1 dhidi ya Brazil kwenye mchezo wa nusu fainali wa kombe la dunia na kufikisha mabao 16. Lilikuwa bao lake la pili katika mashindano baada ya kufunga bao akitokea benchi katika mchezo dhidi ya Ghana,  hatua ya makundi na kumfanya alingane mabao na gwiji wa Brazil. Historia: Shuti lililomfanya ashikilie rekodi ya dunia

HAYA NDIO MANENO ALIYOTAMKA LUIZ FELIPE SCOLARI BAADA YA KUFUNGWA 7-1 NA UJERUMANI

Luiz Felipe Scolari, kocha wa Brazil “Ni wakati mbaya zaidi kuwahi kutokea katika kazi yangu ya ukocha na siku mbaya zaidi katika maisha yangu ya soka. Lakini maisha yanaendelea. Nani anawajibika kwa matokeo haya? Ni mimi, ni mimi. Lawama za matokeo haya mabaya zinaweza kutuhusisha wote, lakini mtu aliyeamua timu ya kucheza na mbinu nilikuwa mimi.

DK. SHEINA FUTARISHA WANANCHI KASKAZINI PEMBA

Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (wa tatu kushoto) akiwakaribisha Mashekhe katika futari  aliyoiandaa kwa Wananchi  waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba huko Viwanja vya Ikulu ya Wete jana.[Picha na Ramadhan Othman,Pemba.] Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba wakijumuika kwa pamoja katika futari iliyoandaliwa na Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,kwa wananchi hao katika viwanja vya Ikulu ya Wete pemba jana. [Picha na Ramadhan Othman,Pemba.] Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (katikati) akijumuika na akinamama   na Viongozi katika Mkoa wa Kaskazini Pemba katika futari aliyowandalia katika ukumbi wa Ikulu ya Wete Pemba jana. [Picha na Ramadhan Othman,Pemba.] Baadhi ya  akinamama mbali mbali wa  Mkoa wa Kaskazini Pemba wakiwa katika futari aliyowandalia na Mke wa Rais Mama Mwanamwema Shein,katika ukumbi

MUDA WA NYONGEZA KWA WAOMBAJI MIKOPO AMBAO HAWAKUJAZA FOMU ZA MAOMBI YA MIKOPO KABLA YA JUNI 30, 2014

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inawafahamisha waombaji wa mikopo kwa mara ya kwanza na Umma kwa ujumla kwamba muda wa maombi ya mikopo umeongezwa kwa mwezi mmoja kutoka Julai 1, 2014 hadi Julai 31, 2014. Bodi ilianza rasmi kupokea maombi ya mikopo kwa njia ya mtandao kuanzia Aprili 23, 2014 ambapo tarehe ya mwisho wa kupokea maombi hayo ilikuwa Juni 30, 2014. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imetoa muda wa nyongeza kwa waombaji wa mikopo kukamilisha maombi ya mikopo katika kipindi cha siku 30, kupitia mtandao kwa anuani: http://olas.heslb.go.tz. Mwombaji wa mkopo atakayekumbana na matatizo ya kiufundi wakati wa kujaza fomu yake apige simu kwenye dawati la msaada la Bodi kupitia namba 022 550 7910 kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa saa 2.00 asubuhi hadi saa 2.00 usiku, na Jumamosi kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 10.00 jioni. Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi hayo kwa njia ya mtandao ni 31 Julai 2014 na hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza

HAYA YA BRAZIL KUPIGWA 7-1 NI MAJANGA, KWA SIMBA SC MUDA WA KUPANGA MAJESHI UMEFIKA, FANYENI HAYA…….

LUIZ Felipe Scolari amekubali kubeba lawama zote kutokana na fedheha waliyoipata Brazil kutoka kwa `watu katili` Ujerumani. Haikutegemewa na wengi kama Brazil wangeingia katika rekodi mbaya ya kombe la dunia kwa kufungwa mabao 7-1 na Ujerumani katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la dunia jana usiku. Brazil waliojiamini, waliingia kwa kasi, lakini bao la mapema la Thomas Muller liliwatoa upepo ghafla ya kufungisha mabao mengi zaidi. Bora Neymar hakuwepo katika mchezo huo. Huyu ni mchezaji mwenye kiwango cha juu kama alivyo kwa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo. Kama angekuwepo uwanjani, halafu Brazil ikafungwa mabao kama ya jana, basi ingemharibu zaidi katika maisha yake ya soka. Tatizo kubwa la Brazil lilikuwa kwenye safu ya ulinzi iliyoongozwa na nahodha David Luiz, Maicon, Marcelo na Dante. Hawa walikuwa tatizo jana, walikaba vibaya, utulivu ulikuwa `F`. Hata Neymar angekuwepo, kwa aina ya uchezaji wake, bado safari ya Brazil ingefika mwisho kwasababu as

HUU NDIO UKWELI KUHUSU BOMU ILIYOLIPUKA ARUSHA

WATU 8 WAJERUHIWA NA BOMU NA Ferdinand Shayo, ARUSHA WATU wanne ambao ni raia wa Asia wamejeruiwa vibaya na kitu kinachiosadikiwa kuwa ni bomu wakati wakila katika Hotel ya Wama iliyopo maeneo ya Gymkhana Jijini Arusha. Tukio hilo limetokea majira ya saa 4 usiku ambapo bomu hilo lililotupwa kwa mkono na  watu wasio julikana na kuwajeruhi watu hao ambapo mmoja amejuruhiwa vibaya na amewekwa katika  chumba cha uangalizi katika Hospitali ya Seliani Arusha. Akizungumza na waandishi wa habari kaimu Mganga mkuU wa hospitali ya seliani Dr Paulo Kisanga alisema kuwa hospitali hiyo iliyopokea majeuhi 8,wanaume 5 wanawake 3 na wamejeruhiwa katika maeneo  miguu na majeruhi mmoja amekatwa mguu mmoja na hali  yake bado ni mbaya. Dr Kisanga aliwataja majeruhi hao kuwani Vinod Sureshi,Rutwik Khamd Val,Raji Rajin,Prateek Saveq,Manc Gumpka,Manisha Gupta,Mahushi Gupta na Deepale Gupta wote walikuwa raia wa Asia. Kwa upande wake mbunge wa jeshi maalumu Mkoa wa Arusha Mh C