Skip to main content

Posts

Showing posts from July 20, 2014

Hichi ndicho ALICHOKISEMA LULU BAADA YA ALI KIBA KUACHIA NYIMBO MPYA

Hivi ndivyo ndege ya Air Algerie AH5017: ilivyoanguka na kuuwa abiria wotee

Abiria wote wa ndege ya Air Algerie waliangamia jangwani Abiria wote na wahudumu wa ndege ya Air Algerie AH5017 waliangamia jangwani. Rais wa Ufaransa Francois Hollande ametangaza kuwa majeshi ya ufaransa yamefaulu kupata mabaki ya ndege lakini hawakuweza kuokoa nafsi hata moja. Aidha rais Francois Hollande ametangaza kuwa majeshi hao wamepata mtambo wa kunukuu sauti ''Blackbox'' huko Mali ilikoanguka ndege hiyo iliyokuwa ikielekea mji mkuu wa Algeria Algiers. Abiria wote wa ndege ya Air Algerie waliangamia jangwani Ndege hiyo ilikuwa imetoka mji mkuu wa Burkina Faso Ouagadougou ikiwa na Abiria 110 na wahudumu 6 . Abiria 51 waliokuwa ndani ya ndege hii walikuwa ni raiya wa Ufaransa. Wengine walikuwa 27kutoka Burkina Faso, 8 kutoka Lebanon , 6 kutoka Algeria , 2 kutoka Luxembourg, 5 kutoka Canada, Wajerumani 4 . Jamaa ya wahasiriwa wanakutana huko Ougadougu Burkina Faso Abiria wengine walikuwa mmoja kutoka mataifa ya Cameroon , Ubeljiji ,Misri Ukraine Us

ISIS yaagiza wanawake wote kukeketwa.

Umoja wa Mataifa umeelezea ghadhabu kutokana na Fatwa iliyotolewa na Kundi la wapiganaji wa Kiislamu wa ISIS ya kuwataka wanawake wote waliozidi umri wa miaka 11 kukeketwa. Afisa wa shirika la umoja wa mataifa nchini Iraq ,Jacqueline Badcock ameonya kuwa agizo hilo la kidini ama Fatwa itawaathiri zaidi ya wanawake milioni nne kati ya umri wa miaka 11-46. Kundi hilo la wapiganaji wa Kiislamu ndilo linaongoza mashambulizi katika maeneo ya Kaskazini mwa Iraq na wao ndio wanaotawala mji wa Mosul. Kundi hilo linalosheheni wapiganaji wa dhehebu la Sunni ndilo linaloendeleza wimbi la mashambulizi katika taifa hilo linalotishia kusambaratika katika ya maeneo yanayotawaliwa na madhehebu. Ukeketaji sio kawaida nchini Iraq. Mapema juma hili, Isisi iliwalazimisha Wakriso katika mji wa Mosul kuondoka na kuandika herufi N kwenye nyumba zao, hatua ambayo imetambuliwa kama kutaifisha mali za Wakristo katika eneo hilo. Kulingana na amri hiyo mpya iliyotolewa chini ya Sharia, , wan

MBASHA AKANA KUMBAKA SHEMEJI YAKE!!

KESI ya ubakaji inayomkabili mume wa Mwimbaji Flora Mbasha ambae ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili Tanzania Emmanuel Mbasha (32), ilitajwa tena July 23 2014 katika mahakama ya wilaya ya Ilala ambapo Mbasha amesomewa tena mashataka yake huku akikubali sentensi mbili tu kati ya nne zilizosomwa.Akisoma hoja hizo mbele ya hakimu Wilbert Luago, mwendesha mashtaka wa serikali Nasoro Katunga alisema May 23 2014 mtuhumiwa alimbaka binti aitwaye  Yerusalemu Boazi (17) ambae ni mdogo wa Flora na kumlazimisha asimwambie mtu yoyote ambapo wakati akitenda kosa hilo mkewe Flora hakuwepo nyumbani.Katunga aliendelea kufafanua kuwa May 25 2014 Mbasha alirudia tena kitendo cha ubakaji baada ya kumuomba binti huyo amsindikize kumtafuta mke wake ambae hakuwepo nyumbani ambapo walipofika Tabata peke yao, Mbasha alimbaka tena binti.Hizo sentensi zote mbili za juu Mbasha amezikana Mahakamani kwa kusema sio kweli.Hata hivyo iliendelea kuelezwa kwamba tukio hilo la ubakaji liliripo

Hizi ndizo sababu zilizomfanya Ray asiende kimzika Baba yake Johari

Tweet 0 MKURUGENZI wa RJ Company, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameshindwa kumzika baba mdogo wa mkurugenzi mwenza wa kampuni hiyo, Blandina Chagula, Clement Kiyenze Chagula. Mzee huyo alifariki katika Hospitali ya Muhimbili kutokana na matatizo ya presha na figo yaliyokuwa yakimsumbua na kuzikwa katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar ambapo wasanii mbalimbali wa filamu nchini walishiriki akiwemo Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete. Alipoulizwa Ray kwa nini hakuhudhuria mazishi hayo, alisema: “Ukweli ni kwamba mimi sipo Dar. Ndiyo maana sijaonekana huko kwenye mazishi, nipo Mwanza katika shughuli zangu za kikazi, tuko pamoja lakini,” alisema Ray ingawa wachungzi wa mambo wanasema kuwa alikuwepo mjini ila ni kutokana na sababu binafsi zao kati yake na Johari ndo maana hakutaka kwenda huku chuchu hans akidaiwa kuhusika.

LAPTOP ILIYOIBIWA IMESHAUZWA ZAMBIA

Mkuu wa manjago alikwenda acha  gari lake lioshwe  sehemu fulani. Aliporudi akagundua haioni laptop yake. Akawapigia askari wake wakaja wakawakusanya waosha magari wote pale jirani na kuondoka nao. Kesho yake asubuhi mkuu akapigiwa simu na Mchepuko wake kumkumbusha kuwa toka jana yake alikuwa kaacha laptop. Mkuu ndio akakumbuka kosa lake akawapigia askari wake na kuwaambia wawaachie wale waosha magari. Askari wakamjibu, 'Mkuu mbona umechelewa? Wote tumeshawapeleka mahakaman maana baada ya kuwahoji usiku kucha wamekubali kuwa waliiba hiyo laptop na wameshaiuza kwa mfanya biashara wa Kizambia.

Madaktari Tanzania walaani miili kutupwa

Chama cha Madaktari nchini Tanzania kimelaani kitendo cha kutupwa kwa viungo vya binadamu nje ya jiji la Dar es Salaam kinyume cha sheria. Rais wa chama hicho, Dk. Primus Saidia ametaka hatua madhubuti zichukuliwe dhidi ya wahusika ikiwemo kupigwa marufuku kwa mtu au taasisi iliyohusika kuendesha shughuli zozote za utafiti kwa kutumia viungo vya binadamu. Dk Primus ameweka bayana kwamba, licha ya fani hiyo ya udaktari kuruhusiwa kutumia viungo vya binadamu katika shughuli mbali mbali za utafiti kwa mujibu wa sheria za kitaifa na kimataifa lakini ameelezea kwamba kitendo hicho kimekiuka haki za binadamu. Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Chama hicho cha madaktari hapa jijini Dar es Salaam, kiongozi huyo ametaka hatua madhubuti zikuchuliwe dhidi ya wahusika ikiwemo kufungiwa. Sakata la kutupwa kwa viungo hivyo kinyume cha sheria katika mji wa Mbweni nje ya jiji la Dar es Salaam siku mbili zilizopita, lilizua taharuki miongoni mwa watu wa kada mbalimb

Hivi hapa ndivyo Viungo vya binadamu vilivyopatikana Tanzania

Viungo vya binadamu vikiwa vimefungwa mafurushi Viungo mbali mbali vya binadamu vimekutwa katika eneo la kutupa taka la Bunju mjini Dar es Salaam katika mazingira ambayo haijafahamika mara moja kuwa viungo hivyo vimetoka wapi. Kwa mjibu wa Afisa mmoja wa polisi ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema viungo hivyo vya binadamu vilivyokutwa ni miguu,vidole ambavyo vilikutwa vikiwa vimefungwa ndani ya mifuko. Hata pamoja na viungo hivyo pia vifaa vya upasuaji vimekutwa zikiwemo glovuzi. Mtu mmoja anashikiliwa kuhusishwa na tukio hilo ambaye ni dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo lililobeba viungo hivyo vya binadamu. Haijafahamika mara moja miili hiyo ya binadamu imetolewa wapi na ilipelekwa eneo hilo kwa lengo gani. Katika miaka ya hivi karibuni Tanzania imekuwa ikikabiliwa na tatizo la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi au Albino ambapo viungo vyao huchukuliwa,japo kuwa viungo hivi vilivyo

UKAWA MSIZIBE MASIKIO; SAUTI ZINAWALILIA

NIANZE safu hii kwa kumshukuru Mungu kwa kutulinda mmoja mmoja na hata taifa letu. Hakika yeye ni mwema. Nikumbushe tu kwamba viongozi wengi wa kisiasa, baadhi ya wananchi, taasisi za kiraia na madhehebu ya dini wanapaza sauti  kuwasihi Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) warejee bungeni. Mwenyekiti wa Ukawa, Freeman Mbowe. Ni wito wa kila mpenda amani kuwataka wajumbe wa kundi hilo kuitikia ombi hilo na kuwaomba waache kuziba masikio kwani sauti ya wengi ni Baraka kwa Mungu. Makundi hayo kwa nyakati tofauti,…

KAMA SIMBA, YANGA HAWAZIKI TABIA HII, MIAKA NENDA RUDI..MAFANIKIO NDOTO ZA MCHANA!

  Kocha mkuu wa Simba sc, Mcroatia, Zdravko Logarusic (wa kwanza kushoto) HAKUNA uchawi  katika soka!. Kabumbu ni mipango na kupita njia sahihi ili kufikia kiwango cha juu. Tanzania ni miongoni mwa nchi `tia maji tia maji` kwenye mipango ya soka. Viongozi na mashabiki wanataka kupita njia ya mkato `short cut` ili kupata mafanikio. Moja ya kosa kubwa wafanyalo watu wengi ni kulifananisha soka letu na mataifa yaliyoendelea (barani Ulaya na Amerika). Utasikia mbona hata Chelsea, Man United, Barcelona wanafukuza makocha?, wanaacha wachezaji?. Kumbe klabu hizi zina mipango na zimekamatwa na wafanyabiashara ambao wamewekeza pesa zao. Hakuna mfanya biashara atayevulimilia hasara. Mtu anainunua klabu kwa mabilioni ya fedha, mfano Roman Abramovich wa Chelsea. Hawezi kuona kocha anavurunda na kumuacha, lazima achukue hatua kwasababu anataka faida.   Pia klabu za Ulaya, mara nyingi kazi ya kocha ni kutengeneza timu kiuchezaji, (ufundi na mbinu za mpira).  kwa asilimia

MWAMBUSI AJIANDAA KUCHEZA `FAINALI 26` LIGI KUU BARA

MSIMU uliopita wa ligi kuu soka Tanzania bara, Juma Mwambusi wa Mbeya City fc alichaguliwa kuwa kocha bora wa msimu baada ya kuiongoza klabu hiyo mpya kushika nafasi ya tatu katika msimamo. Mbeya City fc walizisumbua klabu kubwa za Simba na Yanga, hata mabingwa Azam fc. Walimaliza nafasi ya tatu mbele ya mnyama Simba kwa kujikusanyia pointi 49 kibindoni. Walishinda mechi 13, wakatoka sare mechi 10 na kufungwa mechi 3. Walikula kipigo cha kwanza cha bao 1-0 kutoka kwa Yanga ndani ya uwanja wa Taifa. Wakalala 2-0 dhidi ya Wagosi wa Kaya, Coastal Union, Mkwakwani Tanga. Na mechi ya tatu kufungwa ni ile ya 2-1 dhidi ya Azam fc. Mechi hii ilipigwa uwanja wa Sokoine na kimsingi ndio iliamua ubingwa kutua mikononi mwa wana Lambalamba. Kocha wa Mbeya City fc, Juma Mwambusi (katikati) akizungumza na wachezaji wake Hassan Mwasapili (kushoto) na Peter Richard (kulia). Mwambusi ni kocha maarufu nchini, kila timu anayoifundisha inapata mafanikio. Kumbuka alipokuwa na waje

Sikiliza na kudownload wimbo mpya na ni kali kutoka kwa A BOYZ Feat PNC - Chopolochopolo (Official Audio

DJ Emanuel Msigwa ambaye ni meneja wa kundi la A BOYZ Bad sky na  Jac B ambao ni Wasanii wanounda kundi la Aboyz Bad sky na  Jac B

Watu wengine 4 wauawa Mombasa

Watu wenye bunduki waliokuwa kwenye pikipiki wamewaua takriban watu wanne katika mji ulioko pwani ya Kenya Mombasa. Polisi inasema watu hao walikuwa wakifyatua ovyo risasi kwa wapita njia. Mji huo wa Bandari umeshuhudia ghasia katika miezi ya hivi karibuni huku kukiwepo mashambulio ya mabomu na ufyetuaji wa risasi ambayo wanamgambo wa alshabaab kutoka Somalia wanatuhumiwa kuyatekeleza.

msikilize amani james live kupitia hapa moshonomedia.blogspot.com