Skip to main content

Taasisi 1,200 Duniani Zampa Tuzo ya Amani Edward Lowassa


Taasisi 1,200 duniani zitampa aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa Tuzo ya......... Amani kutokana na utulivu aliouonyesha kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu.

Akizungumza kutoka Bukavu, DR Congo, mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii, Mchungaji William Mwamalanga alisema Lowassa amechaguliwa jana mjini Bukavu na wajumbe 1,400 wa mkutano huo.

Mwamalanga alisema wajumbe wanaohudhuria kongamano la amani wanatoka mataifa ya Ulaya, Marekani, Asia na Afrika kwa kuwashindanisha wanasiasa 1,000 ili kumpata Kiongozi Bora wa Amani mwaka 2015, ambaye anajali na kuangalia maslahi ya jamii badala ya madaraka.

Hatua ya kumpatia tuzo Lowassa ni baada ya kuelezwa kuwa amedumisha amani hiyo hata baada ya kushindwa uchaguzi Mkuu wa Rais Oktoba 25.

Katika uchaguzi uliopita, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)ilimtangaza Dk John Magufuli kuwa mshindi kwa kupata kura 8,882,935 ikiwa ni asilimia 58.46 wakati Lowassa alipata kura 6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote.

Mchungaji Mwamalanga alisema katika kongamano hilo, wajumbe walijadili hali ya amani duniani na mchango wa wanasiasa katika kulinda amani hiyo.

Alisema kuwa wanasiasa barani Afrika wamekuwa vyanzo vya migogoro na mauaji ya raia wakati wa uchaguzi, kama ilivyo nchini Burundi. Hata hivyo, alisema kuwa wajumbe walipongeza ushindi wa Dk Magufuli, lakini wakasema umetiwa dosari na hali ya kisiasa Zanzibar baada ya matokeo kufutwa.

Alisema wajumbe wa kongamano hilo linaloshirikisha maaskofu, masheikh na vijana kutoka madhehebu mbalimbali ya dini barani Afrika, wamemuhimiza Rais Magufuli kumaliza utata wa uchaguzi wa Zanzibar.

Baada ya kupitishwa kugombea urais kwa tiketi ya Chadema, Lowassa alitangaza kuwa angefanya kampeni kistaarabu na kwa amani na baada ya matokeo aliwatuliza wafuasi wa chama hicho, akisema “hakuna anayeweza kuizuia bahati ya mtu” kwa hiyo kama amepangiwa kuwa rais, atakuwa.

Lowassa, ambaye ni Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne, aliongeza upinzani kwenye uchaguzi wa mwaka huu baada ya kuihama CCM na kujiunga na Chadema iliyoukuwa na nguvu ya vyama vingine vitatu vya NLD, CUF na NCCR-Mageuzi.

Kama alivyoahidi, Lowassa hakutumia mikutano yake ya kampeni kushambulia mambo binafsi ya wagombea wengine, bali muda mfupi kuomba kura.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...