Skip to main content

TAMASHA LA MATUMAINI 2013: MASHABIKI MIKOANI WAMIMINIKA DAR!


WAKAZI wa mikoa ya jirani tayari wameanza kumiminika jijini Dar kwa ajili ya kushuhudia Tamasha la Matumaini litakalofanyika Julai 7, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa.
Gumzo zaidi linalozungumzwa na mashabiki hao ambao wengi wao wamesema wanatokea Mikoa ya Morogoro, Tanga, Iringa na Dodoma ni kuwaona wabunge wa Simba na wale wa Yanga watakaposhuka dimbani kucheza soka huku baadhi yao wakishiriki katika mapambano ya..........
ndondi dhidi ya waigizaji.
JB.
Kwenye eneo la ndondi, Mhe. Halima Mdee atapigana na Jacqueline Wolper, Mhe. Zitto Kabwe na Vincent Kigosi ‘Ray’, Mhe. Ester Bulaya atavaana na Aunt Ezekiel huku balaa zaidi likitarajia kuandikwa na mabondia Patrick Amote (Mkenya) atakayevaana na Thomas Mashali (Mtanzania) huku Mkenya Shadrack Muchanje akipigana na Francis Miyeyusho (Mtanzania).
“Nimetoka Tanga hadi Dar kwa ajili ya kushuhudia tukio hili kubwa la historia, navuta picha pale jukwaani nimuone Mhe. Zitto Kabwe akizichapa na Ray na pale wabunge wa Simba watakapojitupa uwanjani kucheza soka,” alisema Ally Juma, mkazi wa Tanga.
Mratibu wa tamasha hilo lenye lengo la kuchangia Mfuko wa Mamlaka ya Elimu nchini (TEA), Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’ amewahakikishia mashabiki waliotoka mikoa ya jirani pamoja na wenyeji, burudani itakwenda kama ilivyopangwa na ulinzi wa kutosha.
“Ni tamasha kubwa, mbali na mechi za wabunge na ndondi, kutakuwa na burudani ya Prezzo, Diamond, Wanaume Halisi, Bendi ya Mlimani Park, Jahazi, Wanaume Family na H. Baba, mechi za mpira wa miguu kati ya Bongo Fleva na Bongo Movie.
“Hayo yote yatafanyika chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi, mbwa, farasi, Ninja zaidi ya 60 na mabaunsa wasiopungua 50. Niwahakikishie mashabiki wataondoka uwanjani salama salmini,” alisema Abby Cool na kuongeza:
“Mwigizaji Jacob Steven ‘JB’ amesema anamhitahitaji Mhe. Idd Azzan kwenye ndondi hivyo kama mbunge huyo ataridhia, watavaana ulingoni ambapo JB ameapa kumtandika mheshimiwa huyo ndani ya sekunde 35.”
Viingilio vya tamasha hilo ambalo pia litahusisha mechi za wanafunzi wa Sekondari za Jitegemee na Makongo, vitakuwa ni shilingi 20,000 kwa V.I.P, 10,000 viti vya bluu na 5,000 viti vya kawaida.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...