Skip to main content

Madiwani waliotimuliwa CCM wadai kuwa wako tayari kuhamia CHADEMA




MADIWANI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliofukuzwa katika Manispaa ya Bukoba, wamesema wako tayari kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kama chama chao kitaendelea na msimamo wa kuwafukuza. 


Akizungumza na................ MTANZANIA kwa njia ya simu jana, mmoja wa madiwani hao ambaye alikataa kutaja jina na kata yake, alisema wako tayari kuhamia Chadema muda wowote kama hawatarudishiwa uanachama wao.

Alisema, madiwani wote waliofukuzwa wana msimamo mmoja ambapo wanasubiri vikao vya Kamati Kuu ya CCM ili wajue hatima yao.

Kwa mujibu wa diwani huyo, wanachokifanya wao ni kutetea maslahi ya taifa na wananchi waliowapigia kura, wala siyo kulinda biashara za watu hata kama wanaungwa mkono na uongozi wa CCM.

Msimamo wa madiwani hao, umekuja siku mbili baada ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, kuwakaribisha Chadema madiwani wote waliofukuzwa katika manispaa hiyo na kwamba kama wakijiunga na chama hicho, watafundishwa siasa za mageuzi.

Mbowe aliwakaribisha madiwani hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Uhuru Mjini Bukoba juzi, katika mwendelezo wa mikutano ya chama hicho ya mabaraza ya wazi yanayojadili rasimu ya Katiba mpya.

Katika mazungumzo yake, Mbowe alikwenda mbali na kusema chama chake kiko tayari kushirikiana na kiongozi wa CCM anayepinga ufisadi kama anavyofanya Mbunge wa Bukoba Mjini, Khamis Kagasheki.

Alipoulizwa kama wamepata mawazo ya kujiunga na Chadema, baada ya kauli ya Mbowe, diwani huyo alisema wao walishakuwa na mawazo hayo, lakini kauli ya mwenyekiti huyo imewaweka huru zaidi.

“Si kama tumeamua sasa, mawazo ya kuhamia Chadema tulikuwa nayo baada ya uongozi wa mkoa kutangaza kutuvua uanachama, lakini kwa kauli ya Mbowe, kutukaribisha rasmi Chadema, ametujengea moyo zaidi.

“Tatizo letu na meya linafahamika kwamba, ni ufisadi wake tulioulalamikia tangu mwaka jana kwenye vikao vya baraza la madiwani, hatukusikilizwa badala yake tunaonekana wasaliti wa chama.

“CCM wanapaswa kujua kwamba, hoja za wapinzani zikiwa sahihi wananchi wanawaunga mkono, vivyo hivyo na sisi hatuwezi kubeza hoja zao kwa sababu tu ni wapinzani, tutaonekana watu wa ajabu.

“Kimsingi, tumefarijika na kauli ya Mbowe, baadhi yetu tulikuwapo katika mkutano wake jana (juzi) pale Uwanja wa Uhuru, ni suala la muda tu mtasikia Bukoba imezaliwa upya,” alisema diwani huyo.

Balozi Kagasheki ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Mjini (CCM), anatajwa kuwa na uhasama wa kisiasa na kada mwenzake, Anatory Amani ambaye awali wawili hao walikuwa na ushirika wa karibu.

Alipotakiwa kuzungumzia suala la kufukuzwa kwa madiwani hao, Kagasheki alisema yeye hakuwepo katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Mkoa kilichowavua uanachama.

Kuhusu taarifa za kutoelewana na Amani, alisema kila mmoja amekuwa na mtazamo wake juu ya mvutano huo.

“Kila mtu ana maoni yake, siwezi kuzuia hisia na maoni ya watu wengine, kila mtu anaweza kutoa maoni atakavyo, ngoja watu waseme,” alisema Kagasheki.

Madiwani wanane waliofukuzwa wanatuhumiwa kushirikiana na wenzao wa upinzani kusaini hati maalumu na kuiwasilisha kwa mkurugenzi wa manispaa, wakimtaka aitishe kikao ili wapige kura ya kumng’oa madarakani Meya Amani.

Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera kilichokaa Agosti 3 mwaka huu, kiliwafukuza uanachama na uongozi madiwani hao akiwamo Mwenyekiti wake wa Wilaya ya Bukoba, Yusuph Ngaiza na Diwani wa Kata ya Kashai.

Wengine waliofukuzwa ni Diwani wa Kata ya Buhembe, Alexander Ngalinda, Samwel Ruhangisa (Kitendaguro), Dauda Kalumuna (Ijuganyondo), Deus Mutakyahwa (Nyanga), Robert Katunzi (Hamugembe), Richard Gasper (Miembeni) na Murungi Kichwabuta ambaye ni Diwani wa Viti Maalumu.


-Mtanzania

Comments

Popular posts from this blog

ANGALIA VIDEO YA MWANAMKE AKIZINI NA CHUPA YA SODA YANASWA

 Katika  hali  ya  kushangaza  na  kuashiria  miisho  ya  dunia, binti  mmoja  amenaswa  " live " akifanya  mapenzi  na  CHUPA YA SODA. Katika  video  hiyo, binti  huyo  anaonekana  akitoa  ushirikiano  wa  kutosha  mithili  ya .............

HUYU NDIYE ALIIYELAZIMISHWA KUFANYA MAPENZI NA MBWA PAMOJA NA FARASI KWA AJILI YA PESA.

When the Internet first came to the continent of  African society,most people were  very pleased with it because it reduces stress of communication with love around the world,it also serve as productive purposes like communication.It served many people for chatting, sending mails and even business. As the time passed by many ladies discovered that they could use the internet to find a chat friend or a life partner.Some girls have greatly benefited just by using the internet to find their dream marriages or relationhsips. Others have fallen into traps in the West and wish they would never have known what the internet was.This is the case of one Cameroonian,Elvire Axelle Tchamakoua. Continue....... SEE HOW IT ALL HAPPEN.... Axelle is pr00stit-te who is pimped to various men by her main man Jean Claude(French Businessman).She did not mind serving her customers from the front or from behind.The use of condoms during her encouters was the allowed as it b

HAYA NDO MANENO YA KUMPANDISHA hisia MPENZI WAKO UMPENDAE!!!!!

                                       Inawezekana wengi wetu tukawa tunayatumia bila kujua kwamba tumekusidia kuyatumia. Haya ni maneno au kauli ambazo mume/mke anaweza mwambia mwenza wake kama ishara ya kumpandisha "nyege" kabla ya kuanza  kufanya mapenzi. Wawili hawa wanaweza wakawa sehemu tofauti tofauti, mfano mume yupo kazini lakini anakaribia kurudi nyumbani, mke ukaanza "kumcharura" mumeo kwa kauli mbali mbali aidha kupitia sms au kwa kumpigia simu, ingawa kupitia sms ndo inasisimua zaidi! Hapa najua naongea na watu wazima, sina haja ya kuandika zaidi maneno yenyewe lakini kila mmoja ni mjuzi wa tabia na vitu ambavyo mwenza wake anavihusudu hasa mkiwa kitandani, mfano" Baby ukirudi leo nataka unipindishe pale katika dressing table kama ulivyonifanyia jana, na leo nimevaa lile gauni ulipendalo na zile bikini mpya, dont be late my love" Maneno haya kwa anayejua mapenzi na anampenda mkewe ni lazima huko alipo "Jogoo" awike kidog