Skip to main content

Yanga, Simba; Ama zao ama zetu

  

 Kikosi cha timu ya Mbeya City mara baada ya kupanda daraja, leo timu hiyo inapambana na Yanga jijini Mbey

SAHAU Manchester United dhidi ya Crystal Palace au Arsenal vs Sunderland. Shughuli ipo Dar es Salaam na Mbeya leo Jumamosi, unaijua?
Simba na Yanga zimetamba kila mmoja kwa kudai ama zao ama zetu, lakini mambo yote yatakuwa hadharani leo Jumamosi.
Vinara wa Ligi Kuu Bara, Yanga kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa msimu mpya wa ligi inatoka nje ya Dar es Salaam na Simba kwa mara ya kwanza inarudi katika jiji lenye Bahari ya Hindi.
Yanga, wanacheza na timu mpya yenye hamasa kubwa ya mashabiki mjini Mbeya ya Mbeya City kwenye uwanja chakavu wa Sokoine huku Simba ikiwa Dar es Salaam kucheza na timu king’ang’anizi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wenye kapeti.
Ingawa Yanga ilikuwa ikifanya mazoezi kwenye uwanja chakavu wa Shule ya Sekondari Loyola, Dar es Salaam, Kocha wake Ernest Brandts alisema: “Nimeuona Uwanja (Sokoine), si mzuri kabisa, sijui mechi yetu itakuwaje.”
Mbali na hilo pia alisema wachezaji wake wana uchovu wa safari, lakini atamkosa kiungo wake mahiri Mnyarwanda Haruna Niyonzima ‘Fabregas’ ambaye hajajiunga na timu tangu alipokwenda kwao Rwanda kuchezea timu ya Taifa.
Brandts alisema: “Nasikitika kumkosa mchezaji muhimu kama Niyonzima pamoja na Hamis Kiiza ingawa wachezaji wengine kama, Ngassa (Mrisho amefiwa na bibi yake) na Lusajo (Realintus yupo chuo) hatupo nao kwenye safari hii ya hapa Mbeya.”
Kwa upande wa Mbeya City, kocha wa timu hiyo, Juma Mwambusi alisema: “Mpira ni dakika 90, timu yetu ni changa na Yanga ni wakongwe, nawaheshimu kwa hilo. Kama kocha nimejipanga kwa upande wangu kuona tunafanya vizuri katika mechi hii.”
SIMBA VS MTIBWA
Simba ambayo ilijificha Bamba Beach, Kigamboni, Dar es Salaam, inacheza na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa.
Mtibwa iliifunga Simba nyumbani na ugenini kwenye mechi za ligi msimu uliopita na wameapa kurudia hilo msimu huu jambo ambalo limeongeza msisimko wa mchezo huo.
Wekundu wa Msimbazi wana mseto wa chipukizi kama, Ramadhani Singano ‘Messi’, Twaha Ibrahim ‘Messi’, William Lucian ‘Gallas’ na Adam Miraji watakaosaidiwa na wazoefu kama, Abdulhalim Humoud ‘Gaucho’, Amri Kiemba, Said Nassor ‘Cholo’ na Henry Joseph anayecheza mechi hiyo kwa mara ya kwanza baada ya misimu mitatu alipokuwa Kongsvinger ya Norway.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...