Skip to main content

DENTI WA KAPUYA AZUA JIPYA


Na Waandishi Wetu
Global Publishers Ltd ilipoamua kufuatilia sakata la denti anayedai kubakwa na Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Juma Athuman Kapuya, lilijua yapo mengi yatajitokeza, Amani lina jipya lingine.

Denti akiwasikiliza wana GPL wakati wa mahojiano
                                       Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Profesa Juma Athuman Kapuya.
Huu ni muendelezo wa utekelezaji wa ahadi ya Global, iliyotoa Jumamosi iliyopita kwenye Gazeti la Risasi kwamba waandishi wake watafuatilia kisha magazeti yake yataandika kila kitu. Katika Ijumaa Wikienda, Kapuya alifunguka, Uwazi liliandika utapeli mzima wa denti husika.
Amani linalo jipya la denti huyo tapeli, Halima Hamad au Felista, aliyeamua kufunguka mbele ya waandishi wetu kwamba ni kweli yeye ni mama wa mtoto mmoja.
Denti akiwasikiliza wana GPL wakati wa mahojiano.
Kuhusu kubakwa, Felista ambaye pia hutumia majina ya Leylat au Leila, alisema: “Kapuya hakunibaka ila nimezaa naye mtoto mmoja.”
                                                 Denti akiwa busy na simu yake wakati wa mahojiano na GPL..
ILIKUWAJE AKAFUNGUKA?
Timu ya waandishi wa habari wa Global Publishers hutekeleza majukumu yake kisayansi, baada ya kurukaruka sana, Felista akidai hahusiki na skandali hiyo na kwamba yeye ni shahidi tu wa mtu anayeitwa Leylat, hatimaye alibanwa kwa maswali magumu, akajikuta akisema ambayo hakuyapanga.
MWANDISHI:  Hizi namba 0753 7…7…28 na 0713 7...20…0 (tarakimu mbilimbili zimefichwa), ni za nani?
FELISTA: Ni namba zangu.
MWANDISHI: Hizi namba ndizo ambazo Kapuya ametutumia  kwamba ndiyo za mtu ambaye huwasiliana naye na humtumia pesa, na ndiye anayejidai ni denti aliyebakwa na kuambukizwa naye Ukimwi.
FELISTA: Siyo kweli, huyo Kapuya anatafuta njia za kujinasua kwenye hili tatizo lake. Anajua mimi namjua Leylat ambaye ndiye denti aliyebakwa.
MWANDISHI: Wewe unaitwa nani?
FELISTA: Naitwa Felista.
MWANDISHI: Unamjua Halima Hamad?
FELISTA: Halima Hamad simjui.
MWANDISHI: Kapuya kasema denti anayedai kubakwa anaitwa Halima Hamad na ndiye mwenye hizo namba ambazo wewe unakiri ni zako.
FELISTA: Nimesema simjui Halima, mimi naitwa Felista. Aliyebakwa ni Leylat, siyo mimi.
                                                              Denti katika pozi

AKUMBUSHWA ALIYOSAHAU
Miaka ya nyuma Felista akitumia mwavuli wa uyatima, aliwahi kuomba hifadhi kwa mmoja wa waandishi wetu wa kike, aliyeishi naye kwa muda mrefu kidogo nyumbani kwake kabla ya kumgundua kwamba ni tapeli, hivyo kuamua kuachana naye.
MWANDISHI: Wewe Felista umesahau kwamba umeshawahi kukaa nyumbani kwangu na kipindi hicho chote, ulikuwa ukiniletea ripoti za shule zenye jina la Halima Humudy. Vilevile ulishawahi kutolewa kwenye gazeti moja la kila siku (halizalishwi na Global), ukiomba msaada kwamba wewe ni yatima, jina ulilotumia ni hilohilo la Halima Humudy.
Hizohizo namba zako, usajili wake wa laini na katika Tigopesa zimesajiliwa kwa jina la Halima Hamad. Haya kataa mbele ya macho yangu!
FELISTA: …. (kimya).
MWANDISHI: Wewe siyo Halima, sema nikusikie.
FELISTA: Ni kweli, Halima Hamad ni mimi, ila hilo jina silitumii sana.
MWANDISHI: Haya sasa, baada ya kukiri Halima Hamad ni wewe, unaweza kutuambia ukweli kuwa wewe ndiye huyo Leylat au Leila unayemtaja.
FELISTA: (Kwa sauti ya chini iliyopoteza ujasiri), ni kweli mimi ndiye mhusika.
MWANDISHI: Sasa kwa nini ulikuwa unakataa?
FELISTA: Nilikuwa sipendi ninyi Global mjue.
MWANDISHI: Haya tuambie ukweli sasa kuhusu wewe na Kapuya.
FELISTA: Nimezaa naye mtoto mmoja.
MWANDISHI: Mbona unatubabaisha? Mara alikubaka, mara umezaa naye mtoto mmoja, ukweli ni upi?
FELISTA: Ukweli ni kwamba yeye ndiye baba wa mtoto wangu.
MWANDISHI: Wewe hujazaa na Kapuya, huu nao ni utapeli mwingine.
FELISTA: Kama hamtaki basi.
MWANDISHI: Kama ni kweli yule ni mzazi mwenzako, mbona unaamua kumchafua na unataka kumharibia maisha yake?
FELISTA: Amekataa kunihudumia ndiyo maana namchafua.
MWANDISHI: Unafikiri hii vita mwisho wake ni nini?
FELISTA: Atakapoanza tena kunihudumia.
MWANDISHI: Haya turudi kwenye pointi ya Ukimwi, kwa nini unamshushia madai mazito kiasi hicho?
FELISTA: Ni kweli nina Ukimwi.
MWANDISHI: Na mtoto wako naye ni mzima?
FELISTA: Mtoto naye ni mgonjwa.
MWANDISHI: Unatumia dawa?
FELISTA: Bado sijaanza kutumia dawa, CD4 zangu bado zipo vizuri.
MWANDISHI: Mbona ulisema mwanzoni kwamba unatumia dawa?
FELISTA: Ni kweli natumia dawa.
MWANDISHI: Mbona unatuchanganya? Mara hutumii dawa, mara unatumia dawa, sasa hivi umesema CD4 zako zipo vizuri.
FELISTA: Nimekwambia natumia dawa. Hata kama CD4 zangu zipo vizuri, natumia dawa hivyohivyo.
MWANDISHI:  Katika maisha yako yote umewahi kupata matatizo ya akili? Maana naona kama haupo sawa.
FELISTA: Mimi ni mzima kabisa. Mtaniona kama ni mzima siku nitakaposimama na Kapuya mahakamani.
MWANDISHI: Wewe Felista umewahi kudanganya unasoma Turiani Sekondari, Mugabe Sekondari na Jangwani Sekondari kumbe ni uongo mtupu.
FELISTA: Nimesoma Turiani tu, sijawahi kusoma Mugabe wala Jangwani.
MWANDISHI: Nimeshawahi kukuona umevaa sare za Jangwani, leo unabisha? Na uliniambia unasoma huko.
FELISTA: Siyo kweli.
MWANDISHI: Kwa nini uliwatapeli Dk. Kimei na Mama Salma Kikwete?
FELISTA: Kuhusu Kimei ni uongo, Mama Salma ni watu walitaka kuniharibia, nikapelekwa Segerea lakini nilitoka.
MWANDISHI: Ilikuwaje ukamtapeli Mama Salma kuwa wewe ni yatima?
FELISTA: Nilitaka nipate nafasi ya kusoma Mkuranga, sasa ili nipate nafasi kule ilibidi nionekane nasoma Jangwani, kwa hiyo nilitengeneza nyaraka zinazoonesha nasoma Jangwani ndiyo baadaye ikaonekana nimefanya utapeli.
MWANDISHI: Umeona sasa? Mwanzoni ulikataa kuhusu kujidai unasoma Jangwani, sasa hivi unakiri. Haya sasa twende tukapime Ukimwi.
FELISTA: Sipimi.
MWANDISHI: Sisi tunaamini hauna Ukimwi. Hata mwanzoni ulishatuthibitishia kuwa ulishapima na upo salama. Kama una uhakika wewe ni mwathirika basi twende tukapime.
FELISTA: Sipimi nimesema.

NI SKANDALI LA VIGOGO
Katika mahojiano hayo, Amani limeweza kubaini kuwa wapo wanasiasa kadhaa ambao wapo nyuma ya Felista na ndiyo wanaompa kampani kwenye harakati zake za kumchafua Kapuya.
Mmoja wa wabunge wa Mkoa wa Tabora (CCM), sauti yake imenaswa mara mbili kwenye simu ya Felista, ya kwanza akimuelekeza binti huyo: “Njoo Dodoma, nitakuitia waandishi wa habari, ufanye mkutano nao uwamwagie kila kitu.”
Sauti nyingine ya mbunge huyo, inasikika ikihoji: “Nimesikia Kapuya anatangaza wewe una watoto wawili, ni kweli?” Felista anasikika akipinga na kusema hana mtoto hata mmoja.
Wapo wanasiasa wengine ambao wamebainika kumuunga mkono Felista, hivyo kuzidi kulifanya ‘saga’ hilo lionekane la kisiasa zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

ANGALIA VIDEO YA MWANAMKE AKIZINI NA CHUPA YA SODA YANASWA

 Katika  hali  ya  kushangaza  na  kuashiria  miisho  ya  dunia, binti  mmoja  amenaswa  " live " akifanya  mapenzi  na  CHUPA YA SODA. Katika  video  hiyo, binti  huyo  anaonekana  akitoa  ushirikiano  wa  kutosha  mithili  ya .............

HUYU NDIYE ALIIYELAZIMISHWA KUFANYA MAPENZI NA MBWA PAMOJA NA FARASI KWA AJILI YA PESA.

When the Internet first came to the continent of  African society,most people were  very pleased with it because it reduces stress of communication with love around the world,it also serve as productive purposes like communication.It served many people for chatting, sending mails and even business. As the time passed by many ladies discovered that they could use the internet to find a chat friend or a life partner.Some girls have greatly benefited just by using the internet to find their dream marriages or relationhsips. Others have fallen into traps in the West and wish they would never have known what the internet was.This is the case of one Cameroonian,Elvire Axelle Tchamakoua. Continue....... SEE HOW IT ALL HAPPEN.... Axelle is pr00stit-te who is pimped to various men by her main man Jean Claude(French Businessman).She did not mind serving her customers from the front or from behind.The use of condoms during her encouters was the allowed as it b

HAYA NDO MANENO YA KUMPANDISHA hisia MPENZI WAKO UMPENDAE!!!!!

                                       Inawezekana wengi wetu tukawa tunayatumia bila kujua kwamba tumekusidia kuyatumia. Haya ni maneno au kauli ambazo mume/mke anaweza mwambia mwenza wake kama ishara ya kumpandisha "nyege" kabla ya kuanza  kufanya mapenzi. Wawili hawa wanaweza wakawa sehemu tofauti tofauti, mfano mume yupo kazini lakini anakaribia kurudi nyumbani, mke ukaanza "kumcharura" mumeo kwa kauli mbali mbali aidha kupitia sms au kwa kumpigia simu, ingawa kupitia sms ndo inasisimua zaidi! Hapa najua naongea na watu wazima, sina haja ya kuandika zaidi maneno yenyewe lakini kila mmoja ni mjuzi wa tabia na vitu ambavyo mwenza wake anavihusudu hasa mkiwa kitandani, mfano" Baby ukirudi leo nataka unipindishe pale katika dressing table kama ulivyonifanyia jana, na leo nimevaa lile gauni ulipendalo na zile bikini mpya, dont be late my love" Maneno haya kwa anayejua mapenzi na anampenda mkewe ni lazima huko alipo "Jogoo" awike kidog