
Na. Mwandishi wetu.
Vijana
wa shule za sekondari nchini wameaswa kuwa mabalozi wazuri pindi
watakapomaliza masomo yao juu ya kuhamasisha utekelezaji wa malengo ya
milenia kwa sababu ni dira ya maendelo ya taifa na dunia kwa ujumla.
Akizungumza
na wanafunzi wa shule ya Wasichana Kibosho, Lyamungo na Umbwe sekondari
hivi karibuni, Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa,
Bi. Usia Nkhoma Ledama amesema malengo ya milenia yanagusa Nyanja zote
za maendelo kwa vijana walio na wasio mashuleni.
Bi.
Nkhoma amewataka wanafunzi wafanye kazi za kujitolea na kuhakikisha
wanapeleka elimu waliopata kupitia vilabu vya Umoja wa Mataifa kwa jamii
na kuhamasisha dhana ya kujitolea kwa maslahi ya nchi.
“kila
ndani ya saa moja tuna vijana 50 ambao wanapata maambukizi ya VVU kati
ya miaka 14-24 ambao wengi kati ya hao ni Wasichana, hivyo msijihusishe
na masuala ya mapenzi mnapokuwa mashuleni”, amesema Bi. Nkhoma.






Comments
Post a Comment