Skip to main content

HIVI NDIVYO MSANII BONGO MOVIES ALIVYOJINYONGA

Stori: MUSA MATEJA na Imelda Mtema
SAKATA la kujinyonga kwa msanii wa filamu Bongo, Victor Peter limegubikwa na matukio tofauti ya kustaajabisha ambayo marehemu aliyafanya siku kadhaa kabla hajapatwa na umauti, Ijumaa limefukunyua kila kitu.
Mwili wa marehemu Victor Peter ukipelekwa mochwari.
Kwa mujibu wa rafiki wa marehemu, Hamisi Koba, msanii huyo alijinyonga usiku wa Februari 27, mwaka huu mkoani Tanga ambapo marehemu alifika jijini humo kuigiza filamu yake iitwayo Our Family.
Hamisi alisema Victor aliwasili jijini humo akiwa na timu ya wasanii sita na kufikia kwenye nyumba ya kulala wageni iitwayo Safari Junior iliyopo maeneo ya Kisosora ambapo punde walianza kushuti filamu hiyo ambayo yeye na Mzee Jengua ndiyo walikuwa wahusika wakuu.
Marehemu Victor Peter enzi za uhai wake.
“Mimi ndiye nilikuwa kama mwenyeji wake mkubwa hapa Tanga, alikuwa ni mpole na siku zote tulipokuwa kazini kwa ajili ya kushuti filamu hiyo aliniambia mambo mengi kuonesha amejipanga kuhakikisha anaifikisha mbali.
“Victor alitokea Mwanza, akaenda Dar ambapo alifika na kuandaa filamu yake ya kwanza aliyoiita Chozi ambayo tayari ilikuwa imekamilika na kuiuza kwenye Kampuni ya Kapiko ya jijini humo,” alisema Koba na kuongeza:
“Filamu hiyo ilikuwa bado haijatoka, akaamua kuja Tanga kuandaa filamu hiyo ya pili ambayo nayo ilikamilika juzi. Naumia sana ninapokumbuka mipango yake maana alikuwa ana ndoto za kufanya makubwa.
Wasanii wenzake na marehemu wakilia kwa simanzi.
“Siku ya Januari 27 tulipokuwa tunakamilisha filamu, kuna muda alikuwa anaonekana kama ana wenge hivi... alipomaliza kushuti sehemu yake tulienda benki, akachukua fedha na kuwalipa wasanii wote.”
Akiendelea kutiririka juu ya tukio hilo, Koba alisema marehemu alionesha kama alikiona kifo chake kabla kwani aliuliza mara mbilimbili kama kuna mtu anamdai ili amlipe.
“Wakati anatupatia fedha kila mara alikuwa anauliza kama kuna mtu anamdai hadi tuliingiwa wasiwasi na ingawa wengine walisema atakuwa amefurahia labda kumaliza muvi yake,” alisema.
Koba alizidi kueleza kuwa, marehemu akiwa na furaha ya kumaliza muvi hiyo, alikwenda chumbani kwake na kujifungia lakini alfajiri (Januari 28) walipomgongea mlango waligundua amejinyonga.
Baadhi ya mashuhuda wakiwa eneo la tukio.
“Tulichungulia kupitia tundu la funguo tukaona kama ananing’inia ndipo tukaenda kwenye kituo cha Polisi cha Chumbageni na kuchukua askari ambao walishirikiana na mwenye gesti hiyo kuvunja
mlango na kumkuta kajinyonga, tukachukua mwili na kuupeleka kwenye Hospitali ya Bombo, mipango ya kuusafi risha mwili kwenda Kahama nyumbani kwao imeanza,” alisema Koba na kuongeza:
“Kwenye hiyo filamu yake, stori ilikuwa mzee Jengua kama baba wa Victor ambapo Mzee Jengua alikufa na baadaye Victor anakufa kiajabu, kifo kimempata kweli.”
Kuhusiana na kifo hicho, Koba alisema kilimuuma kwani alikilinganisha na kile kilichomtokea marehemu Steven Kanumba ambaye pia aliigiza filamu ya Power of Love ikionesha anakufa, akafa kikwelikweli.
Mwili wa marehemu uliokuwa umehifadhiwa katika Hospitali ya Bombo ulitarajiwa kusafi rishwa juzi kwenda nyumbani kwao Kahama kuzikwa.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...