Skip to main content

Hizi ndizo Sababu za Man Utd kumuuza Rooney



 


MANCHESTER, ENGLAND
MREMBO Coleen Rooney anasubiri kwa hamu kubwa mazungumzo ya mkataba mpya wa mumewe, Wayne Rooney wa kuendelea kubaki klabu Manchester United. Taarifa zinabainisha kwamba mchezaji huyo anaandaliwa mshahara wa pauni 300,000 kwa wiki.
Mrembo huyo anadaiwa kumtaka mumewe asaini mkataba mwingine wa miaka mitano wa kubaki Manchester ili kuwasubiri watoto wao; Kai, 4, na Klay mwenye umri wa miezi minane kuwa na umri mkubwa kabla ya kuhama.
Mkataba ambao Manchester United inataka kumpa Rooney una thamani ya pauni 65 milioni na utamfanya straika huyo kuwa mchezaji anayelipwa pesa nyingi zaidi England.
Kwa sasa analipwa kiwango sawa na mchezaji mwenzake wa Manchester United, straika wa Kidachi, Robin van Persie, pauni 250,000 kwa wiki.
Rafiki wa mrembo Coleen, 27, anasema: “Kitu kikubwa Coleen hataki wahame kutoka Kaskazini Magharibi na jambo hilo ni muhimu sana kwa Wayne. Hataki kuondoka eneo hilo na kutokana na kupokea ofa nzuri ya pesa nyingi anaamini hilo ni jambo muhimu akabaki klabu hapo.”
Manchester United imeipiga marufuku Chelsea kwamba isithubutu kumfuatilia straika wao huyo kwa sababu hawawezi kumuuza kwa wapinzani. Real Madrid pia inafukuzia saini ya staa huyo wa Old Trafford.
Lakini, Coleen hayupo tayari kuona watoto wake wakihamia London wangali wadogo hivyo, ukiweka kando Hispania. Anachotaka yeye waendelee kubaki Manchester hadi hapo baadaye.
Familia hiyo inaishi Prestbury, Cheshire, na wazazi wa Coleen, Colette na Tony wanaishi umbali wa maili 50 huko Formby, Merseyside, karibu na familia ya akina Rooney.
Coleen amesema Rooney, ambaye alijiunga na Manchester United akitokea Everton mwaka 2004, atapata shida sana kutulia kama atacheza bila ya sapoti ya familia zao.
Lakini, kuna mtazamo tofauti wakati kocha David Moyes akihaha na kuafiki mshahara wa pauni 300,000 kwa Rooney, wachambuzi wa soka wanadhani Manchester United inapaswa kulichukulia kwa hadhari suala la mchezaji huyo.
Staa huyo tayari anaonekana kuiringia Manchester United kwa kuweka kando suala la kusaini mkataba mpya akisubiri hatima ya klabu mwishoni mwa msimu kama itakuwa ndani ya nne bora na kama klabu hiyo itafanya usajili wa mastaa wapya.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...