Skip to main content

SERIKALI YATOA UFAFANUZI TAARIFA ZA MAGAZETI JUU YA HOTUBA YA KATIBU MKUU KIONGOZI

sefue
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
ngaoWIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Katika baadhi ya magazeti ya leo tarehe 27 Juni, 2014 yameandika taarifa ambazo sio sahihi likiwemo gazeti la  Uhuru lenye kichwa cha habari “BILA KUPITIA JKT HAKUNA AJIRA SERIKALINI na gazeti la Tanzania Daima lenye kichwa cha habari “IKULU: RUSHWA YA NGONO IMEKITHIRI SERIKALINI”.
Magazeti yote haya yameandika habari za kupotosha Umma kuhusu hotuba ya Katibu Mkuu Kiongozi aliyoitoa tarehe 26/6/2014 katika mkutano wa Mwaka wa Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Makatibu Tawala uliofanyika mjini Dodoma. Magazeti hayo yamejenga taswira kwamba Katibu Mkuu Kiongozi alitoa taarifa kwamba “Hakuna ajira bila kupitia Jeshi la Kujenga Taifa” na “Rushwa ya ngono imekithiri Serikalini”.
Serikali inapenda kutoa ufafanuzi kwamba taarifa hizo siyo za kweli wala hazielezi taarifa halisi aliyoigusia Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi Ombeni Sefue. Katika hotuba yake alisema “Aidha, ningependa mjue kuwa kuanzia sasa tutaweka mkazo mkubwa sana kwenye sifa ya uzalendo kwenye ajira Serikalini.  Hatuwezi kuwa na Watumishi wa Umma ambao hawana uzalendo.Pale ambapo waombaji kazi kwenye Utumishi wa Umma wana sifa zote sawa, lakini wakawepo wale ambao wamepitia Jeshi la Kujenga Taifa watapewa kipaumbele.lakini narudia, kipaumbele hicho kitumike pale tu ambapo sifa zingine zote ziko sawa, na si vinginevyo”. 
Kuhusu suala la rushwa ya ngono lililoripotiwa na gazeti la Tanzania Daima, si kweli kwamba Katibu Mkuu Kiongozi alisema kumekuwa na ongezeko au kukithiri kwa rushwa ya ngono katika utoaji wa ajira serikalini. Alichokisema Katibu mkuu kiongozi ni kwamba “Lakini bado malalamiko yanasikika kuwa ati huwezi kuajiriwa kwenye Utumishi wa Umma isipokuwa kama unajulikana au unatoa rushwa, ama ya fedha au ya ngono.  Jambo hilo linanisononesha sana.  Mimi naamini mambo hayo yamepungua sana.  Lakini kama yanafanyika, ni kinyume kabisa na Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma na lazima tulio katika ukumbi huu tuyapige vita kwa bidii zote, bila kuoneana haya, hadi wananchi waone kuwa kweli hayapo.  Tusipuuze hata kidogo malalamiko ya wananchi, bali tujichunguze na tuchunguzane, ili kama mambo hayo bado yapo, kwa pamoja tuazimie kuyakomesha kabisa kwenye Utumishi wa Umma”. Hotuba halisi ya Katibu Mkuu Kiongozi inaweza kupatikana

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI – MAELEZO
27/6/2014

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...