Skip to main content

Watoto waishio kwenye mazingira magumu hususani wanaoishi na VVU wazidi kunyanyapaliwa.


Mahmoud Ahmad,Arusha.
WATOTO waishio kwenye mazingira magumu  na yatima hususani wanaoishi na virusi vya ukimwi wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya kunyanyapaliwa na wazazi na hata walimu mashuleni hali ambayo imekuwa ikiwawia vigumu watoto hao kuendelea na masomo.Aidha unyanyapaa kwa watoto yatima wanaoishi na virusi vya ukimwi imekuwa ni changamoto kubwa kwao ambapo asilimia kubwa ya watoto wamekuwa wakikosa haki zao za msingi hususani elimu kutokana na hali hiyo.
Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi wa shirika la Sorode Organization la jijini hapa, Sophia Justine wakati akizungumza na watoto na walezi waliohudhuria katika harambee ya kuchangia bweni  kwa ajili ya watoto yatima wa kike  wanaolelewa katika kituo cha Faraja ambapo shs 1 milioni zilipatikana huku zikihitajika shs 50 milioni.
Alisema kuwa, kumekuwepo na unyanyapaa wa hali ya juu unaofanywa na walimu katika  shule mbalimbali baada ya kupewa taarifa kuhusu watoto hao hali ambayo imekuwa ikisababisha watoto hao kutengwa na wengine na hata wakati mwingine kuchukiwa kabisa na walimu na wazazi kwa ujumla.
Sophia alisema kuwa, watoto hao wanahitaji  kupatiwa haki zote za msingi kama wanavyopata watoto wengine badala ya kunyanyapaliwa na kutengwa na jamii kama watoto wasiofaa na kustahili kama wengine kitendo ambacho kimekuwa kikiwapa wakati mgumu kuishi katika jamii.
‘sisi shirika letu hili tumekuwa tukitoa elimu kwa jamii mbalimbali ikiwemo vituo mbalimbali vya watoto yatima ili kuweza kujua haki za mtoto ,na changamoto zinazowakabili ndio maana leo tukaamua kuandaa harambee hii ambayo ndo mwanzo tu lengo ni kuhakikisha fedha za bweni  zimepatikana kwa ajili ya kusaidia watoto hawa wa kike’alisema Sophia.
Naye Mkurugenzi wa kituo hicho cha kulelea watoto yatima cha Faraja ,Faraja Maliaki alisema kuwa, kituo hicho kina jumla ya watoto 200 ambapo kati ya hao watoto 30 wanaishi na virusi vya ukimwi na  watoto 48 wakiwa hawajulikani kabisa walipotokea wala makabila yao kutokana na kuokotwa baada  ya kutupwa  baada ya kuzaliwa.
Alisema kuwa, kituo hicho kimekuwa kikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya ukosefu  wa bweni la wasichana ambapo kituo kina idadi ya wasichana 103 ambao wamekuwa na uhitaji huo wa bweni.
Faraja aliongeza  kuwa, watoto hao wamekuwa wakilala chini na wengine kusongamana kwenye kitanda kimoja kutokana na kutokuwa na bweni ,hivyo aliomba wadau mbalimbali kujitokeza kuchangia bweni la watoto hao ambao wanaendelea kukua siku hadi siku.
Aidha alielezea changamoto nyingine kuwa ni pamoja na malazi, chakula,mavazi,kwani wakati  mwingine wamekuwa wakila mlo mmoja tu kwa siku huku idadi yao ikiendelea kuongezeka kila siku

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...