Msanii huyo aliyetamba katika uigizaji akiwa na
Dude katika kipindi maarufu cha Bongo Dar es
Salaam, kwa muda wa miaka saba na baadaye
kuingia kwenye filamu alikuwa akiugua ugonjwa wa
moyo, kiasi cha kumfanya arejee nyumbani kwao
kwa ajili ya matibabu, ambayo hata hivyo,
yameshindwa kunusuru uhai wake.
Kwa mujibu wa GPL, kifo hicho kimeibua hofu upya
kwa wasanii wa Bongo Muvi, hasa ikikumbukwa
kuwa mchunguji mmoja (jina tunalihifadhi) aliwahi
kutabiri kuwa, wimbi hilo la vifo litaendelea tena
mwaka huu kwa wasanii na watu wengine maarufu,
wakiwemo wanasiasa hivyo kuwataka kumrudia
Mungu.
Wasanii kadhaa waliozungumza na Gazeti la Ijumaa
baada ya taarifa za msiba huo walionesha hofu ya
kifo waliyonayo lakini wengi wakasema Kifo cha
Tino ni mipango ya Mungu hivyo kila mmoja
ajiandae tu.
Msanii aliyewahi kufanya kazi kwa karibu na Tino,
Kulwa Kikumba ‘Dude’ alisema: “ Dah! Ni kweli
jamaa katutoka, kikubwa tumuombee na hilo la hofu
ni vyema kila mmoja akawa nayo ili aweze
kujiandaa kwa safari.”
Katika kuonesha kuweweseka, msanii mwingine wa
filamu, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ alisema: “Mimi
sitakufa kwa kuwa niko karibu na Mungu,
watakaokufa ni wale walio mbali na Mungu.”
Msanii mwingine, Isabela alisema kifo cha Tino
kimemshtua mno na kusema ni mapenzi ya Mungu,
lakini akaponda utabiri wa mchungaji akisema
hajawahi kuamini mambo hayo, kauli ambayo pia
ilitolewa na Rose Ndauka.
Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, kulikuwa
hakuna taarifa rasmi zilizotolewa juu ya mazishi ya
msanii huyo.Mungu Ilaze roho ya Marehemu mahali
pema peponi. Amina- Mhariri
Imeandikwa na Hamida Hassan, Gladness Mallya na
Deogratius Mongela
PICHA: Tino enzi za uhai wake.
Comments
Post a Comment