Skip to main content

Lipumba Amtwika Zigo Dr Shein Mgogoro Zanzibar....Asema Mgogoro Utakwisha Iwapo Dr Shein Atakubali ZEC Iendelee Kutangaza Matokeo


Mwenyekiti wa zamani wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ndiye mtu pekee mwenye uwezo wa.............. kumaliza mgogoro wa Zanzibar.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Profesa Lipumba alisema mgogoro wa Zanzibar utamalizwa kwa Dk Shein kuiruhusu Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25.

Alisema pamoja na mazungumzo yanayoendelea kati ya CUF na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk Shein ndiye mwenye uwezo kuumaliza mgogoro huo.

“Mazungumzo yanaendelea na hatujui yatafika mwisho lini, lakini Dk Shein ndiye anayeweza kuifanya Zanzibar iwe na amani au vurugu, ninashauri aruhusu kutangazwa kwa matokeo,” alisema.

Alisema amani na utulivu uliopo Zanzibar wakati wananchi wakisubiri hatima ya mgogoro huo, haiwezi kuwa ya kudumu kwani ikiamuliwa uchaguzi urudiwe wapo ambao hawatakubali.

Profesa Lipumba alisema uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa huru na haki na hata watazamaji wa kimataifa kutoka nchi mbalimbali walishangaa matokeo yake kufutwa.

Alisema wananchi wa Zanzibar walishapiga kura na kwamba wanachosubiri ni matokeo vinginevyo haki yao ya kidemokrasia itakuwa imechezewa.

Oktoba 28 mwaka huu, Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha alifuta uchaguzi huo kwa kile alichosema kulikuwa na kasoro ndani ya tume yenyewe na kwenye vituo vya kupigia kura.

Profesa Lipumba alisema mgogoro huo ukiendelea, utakwamisha msaada wa Dola za Marekani 472.8 milioni uliokuwa utolewe na Shirika la Maendeleo ya Milenia (MCC) la Marekani.

Alisema Bodi ya MCC ilikutana Desemba 16 na kushindwa kupitisha msaada huo kwa Tanzania huku hoja kubwa ikiwa kufutwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu Zanzibar.

Alisema miongoni mwa matumizi ya msaada huo ilikuwa kuunganisha wateja wapya 300,000 kupata umeme.

“Hapa tunategemea busara za Dk Shein kuumaliza mgogoro ili tupate msaada huo wenye masilahi ya Taifa au kuendelea na mgogoro na kuukosa msaada huo,” alisema.

Akizungumzia suala hilo, Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Magdalena Sakaya alisema huu ni muda mwafaka kwa Dk Shein kuweka masilahi ya Wazanzibari mbele.

Alisema atawekwa kwenye vitabu vya historia kama atafanya uamuzi wa kuruhusu kutangazwa kwa matokeo hata kama viongozi wenzake wa CCM hawatapenda uamuzi huo.

“Lakini vurugu zikitokea, Shein atalaumiwa jumuiya za kimataifa yeye mwenyewe na atashangaa viongozi wenzake wa CCM watakapojiweka pembeni,” alisema.  

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...