Skip to main content

Magufuli Aitaka TRA Kutoa Mashine za EFDs Bure.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli, ameishangaa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kwa kutogawa bure Mashine za EFDs, na wao kubaki na kazi ya kukusanya mapato.

Akizungumza katika mkutano wa wafanyabiashara na wawekezaji jana jijini Dar es Salaam, ulioandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) na Baraza la Biashara la Taifa (TNBC), alisema muda uliopotea na kodi ambayo haikukusanywa wakati wa mvutano na wafanyabiashara ungetosha kununua mashine mpya na kuwagawia.

“Kama mnajua mashine hizi ni halali na ni zenu, wapeni bure kazi yenu iwe ni kukusanya kodi, ni hesabu rahisi sana isiyohitaji kwenda chuo kikuu kuwa muda uliopotea na fedha hazifiki bilioni 12 zingetosha kununua na iwe kazi ni kukusanya kodi,” alisema.

Awali katika salamu zake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara, Jonson Minja, alimpongeza rais kwa kazi kubwa aliyofanya Bandarini na TRA kwa kuwa imewezesha kodi kukusanywa kwa usahihi na kwamba kipindi cha nyuma fedha nyingi zilipotea, kutokana na mfumo wa ukusanyaji kodi kutowekwa wazi.

Aidha, alisema mashine za EFDs zitatumika kwa wafanyabiashara wote mwakani, kwa kuwa changamoto zilizosababisha mvutano baina yao na serikali zimemalizika.

Aidha, alimtaka rais kufuatilia kwa karibu ukwepaji kodi katika sekta isiyo rasmi na kwamba kukiwa na mipango madhubuti serikali itaweza kupata kodi kwa wananchi wote.

“Kasi ya rais inatupa matumaini makubwa sana, tunachoweza kusema, Mungu akubariki akupe hekima na nguvu...tunaomba uimarishe viwanda vya kati na vidogo ili malighafi zisisafirishwe kwenda nje, bidhaa ambazo zitasaidia kukuza uchumi na kuimarisha shilingi dhidi ya Dola ya Marekani,” alisema.

Tangu mwaka juzi kulikuwa na mvutano mkali baina ya wafanyabiashara na TRA, ambao waligoma kutumia mashine hizo hadi serikali itakaposhughulikia kero zao ikiwamo bei ya mashine, utitiri wa kodi, ukwepaji kodi na urasimu uliopo.

Wafanyabiashara kwa umoja wao waliitisha mgomo nchi nzima na kumekuwa na mazungumzo ya mara kwa mara na serikali, ambayo wakati mwingine hayakufikia ukingoni, hatua iliyofanya baadhi ya viongozi wa wafanyabiashra kukamatwa.

Minja alikamatwa na Polisi mkoani Dodoma mwaka jana, na kuswekwa ndani, jambo lililofanya wafanyabiashara kuitisha mgomo wa siku tatu hadi serikali itakapoeleza alipo kiongozi wao.

Baadaye ilibainika anashikiliwa na Polisi mkoani humo, na alipandishwa mahakama ya mkoa na kusomewa mashtaka ya kuchochea mgomo wa wafanyabiashara nchini.

Baadaye mahakama ya mkoa ilimuachia huru kiongozi huyo.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...