Skip to main content

Ikulu Yamjibu Dk Makongoro Mahanga Aliyemtuhumu Rais Magufuli Kuunda Serikali Kubwa Tofauti Na Alivyoahidi


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue amesema ameshangazwa na kauli ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongo  Mahanga kuwa wingi wa makatibu wakuu unakinzana na dhana ya kupunguza ukubwa wa Serikali alioahidi Rais John Magufuli.

Juzi mbunge huyo wa zamani wa jimbo la Segerea (CCM) alisema kuteua makatibu wakuu 27 ni sawa na kuwa na wizara 27 badala ya 15 kama inavyoelezwa.

Dk Mahanga alisema huko si kupunguza ukubwa wa Serikali bali ni kuongeza ukubwa wake na kwamba wizara ni ofisi ya katibu mkuu na si ofisi ya waziri.

Lakini, Balozi Sefue alipotafutwa kutoa ufafanuzi kuhusu madai ya Dk Mahanga, alisema kauli ya kiongozi huyo imemshangaza.

“Kwa mtu aliyekuwa naibu waziri kwa muda mrefu sana, inashangaza hajui kuwa makatibu wakuu si sehemu ya Baraza la Mawaziri,” alisema Sefue.

“Idadi yao si kipimo cha ukubwa au udogo wa Baraza la Mawaziri,”alisema Balozi Sefue.

Sefue aliongeza kuwa idadi ya makatibu wakuu na naibu wao waliokuwapo kwenye Serikali iliyopita na waliopo sasa ni tofauti, kwa kuwa wamepungua.

“Jumla ya makatibu wakuu na naibu makatibu wakuu wa Serikali iliyopita ilikuwa 54. Hivi sasa wako 49 tu,” alisema Sefue.

Ikumbukwe kuwa baada ya kupunguzwa kwa Baraza la Mawaziri kutoka mawaziri 55 wa baraza lililopita hadi mawaziri 34 wa baraza la sasa, hata nafasi za makatibu wa wizara zimepungua pia.

Rais alisema makatibu ambao hawajateuliwa, watapangiwa kazi nyingine.

Kauli ya Dk Mahanga, ambayo  aliituma kwenye ukurasa wake wa facebook, iliibua mjadala kwenye mitandao ya kijamii baada ya wananchi kugawanyika, baadhi wakimuunga mkono na wengine wakimkosoa.

Comments

Popular posts from this blog

VIDEO YA NGONO YA WANAOSADIKIKA KUWA NI WANAFUNZI WA IFM YAVUJA

Watu wawili wanaosadikika ni wanachuo wa IFM wajirecord video wakifanya ngono ndani ya........... chumba ambacho kinaonesha kama ni cha hosteli, fungua na uone upuuzi uliofanyika humu ndani…. KUANGALIA VIDEO HII LAZIMA UWE NA UMRI WA ZAIDI YA MIAKA 18+ KUANGALI BOFYA HAPA

Huyu Mzee Ndio Aliyetia Aibu Kwenye Bar Hii yenye Makahaba wanaocheza Nusu Uchi

 vijimambo kwenye bar zetu  

HUYU HAPA NDIYE MCHUNGAJI ADAI KUWAUA KANUMBA NA SHARO MILIONEA, AELEZEA JINSI ALIVYOFANYA....WAUMINI WAPIGWA NA BUTWAA..

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na Steven Kanumba ‘ The Great’ . Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda. VIFO MILIONI 605  Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini. Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao. WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kun...